| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Afrika Kusini 'kuwaheshimisha' wanajeshi 'waliorudi na ujauzito'
Wanajeshi hao walikuwa sehemu ya Jeshi la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) walioko nchini DRC.
Afrika Kusini 'kuwaheshimisha' wanajeshi 'waliorudi na ujauzito'
Siku ya Jumatatu, Jeshi la Ulinzi la Afrika Kusini (SANDF) lilitangaza hatua ya kuwarejesha nyumbani askari majeruhi, pamoja na askari wawili waliopata ujauzito./Picha: SANDF / Others
26 Februari 2025

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Masuala ya Haki na Ulinzi ndani ya Bunge la Afrika Kusini Jane Mananiso, amewapongeza wanajeshi wawili wa kike wa jeshi hilo ambao wamepata ujauzito licha ya kushiriki shughuli ya kulinda amani nchini DRC.

Mananiso alisisitiza kuwa hakuna aibu yoyote kushika mimba katika taaluma yoyote ile, wakiwemo wanajeshi na askari polisi wa Afrika Kusini.

“Si aibu kupata ujauzito, kimsingi ni haki ya kikatiba kwa mwanamke yeyote yule kushika mimba kwa wakati wanaotaka. Kama kamati, tunataka wanajeshi wetu wafanyiwe vipimo sahihi vya ujauzito wanapotumwa kwa shughuli za kulinda amani,” alisema Mananiso.

Aliongeza: “Hili lifanyike ili kuhakikisha kuwa wanapata matunzo mazuri wakati na baada ya ujauzito. Tunajisikia fahari na wanajeshi wetu hasa katika shughuli ya ulinzi wa amani huko DRC.”

Siku ya Jumatatu, Jeshi la Ulinzi la Afrika Kusini (SANDF) lilitangaza hatua ya kuwarejesha nyumbani askari majeruhi, pamoja na askari wawili waliopata ujauzito.

Wanajeshi hao walikuwa sehemu ya Jeshi la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) walioko nchini DRC.

Hali kadhalika, Mananiso amevitaka vyombo vya habari kuheshimu mipaka na kuwapa nafasi ya kupona majeruhi hao.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Afrika Kusini yaomba utulivu kufuatia maandamano dhidi ya kusimikwa kwa 'Igwe' wa Nigeria
Rwanda ‘yahofia’ operesheni za DRC dhidi ya kikundi cha FDLR
Kenya yalipa ada ya Dola milioni 30 ya uenyeji wa AFCON 2027
Hasara ya mamilioni kufuatia ubomoaji katika soko kubwa zaidi la wazi la Gikomba Nairobi
Shabiki maarufu ‘Lumumba Vea’ akosa viza ya  kwenda kuishangilia DRC dhidi ya Jamaica
Mamlaka ya uchukuzi Kenya yazindua ukaguzi wa lazima wa afya kwa madereva ili kupunguza ajali
Tanzania yahimiza matumizi ya AI kuimarisha mtangamano na maendeleo EAC
Kundi lenye silaha limewaua watu wasiopungua 20 Jimbo la Plateau nchini Nigeria
Wafungwa wasiopungua 11 wafariki kutokana na mlipuko wa kipindupindu katika jela DRC
Kagame awaamuru maafisa waandamizi wa serikali 'kusimama' wakati wa hotuba yake
Wadukuzi wadukua maombi ya kazi 450,000 nchini Afrika Kusini
Rais wa Misri asema ni Trump pekee anaweza kusimamisha vita, aonya kupanda zaidi kwa bei ya mafuta
Togo yatoa uzoefu wa kupambana na magonjwa yasiyopewa kipaumbele
Watu 15 wamefariki katika ajali ya barabarani mkoa wa kati Kenya
Mahakama kuu ya Jamhuri ya Congo imethibitisha ushindi wa Sassou Nguesso kwa awamu ya tano
Rwanda, Burundi wanagombana juu ya juhudi za rais wa zamani wa Senegal Sall kuongoza UN
Vifo kutokana na mafuriko nchini Kenya vyaongezeka hadi 108, polisi wasema
Majenerali wakuu wa Uganda wazuiliwa kwa madai ya ufisadi: ripoti
Eswatini yamrudisha nyumbani mwananchi wa Cambodia aliyefukuzwa kutoka Marekani
Waasi waanza kuondoka katika vijiji vya DRC ili kuhimiza amani