| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Watu 6 wafa kwa ugonjwa wa Marburg nchini Rwanda
Taarifa hiyo inakuja baada ya Wizara ya Afya ya nchi hiyo kutangaza siku ya Septemba 27 kuwa ugonjwa huo uliripotiwa katika vituo mbalimbali vya afya nchini humo.
Watu 6 wafa kwa ugonjwa wa Marburg nchini Rwanda
Waziri wa Afya wa Rwanda, Dkt Sabin Nsanzimana./Picha: Wengine / Others

Watu sita wamethibitishwa kufa nchini Rwanda kutokana na kuugua maradhi ya Marburg, Waziri wa Afya wa nchi hiyo, Dkt Sabin Nsanzimana amesema.

“Homa kali inayosababishwa na Marburg imegundulika nchini Rwanda. Jumla ya watu 20 wameugua na wengine sita wamepoteza maisha,” alisema Nsanzimana kupitia video iliyowekwa kwenye ukurasa wa Shirika la Habari la Rwanda (RBA).

Taarifa hiyo inakuja baada ya Wizara ya Afya ya nchi hiyo kutangaza siku ya Septemba 27 kuwa ugonjwa huo uliripotiwa katika vituo mbalimbali vya afya nchini humo.

Kulingana na Nsanzimana, wengi waliopoteza maisha na waliougua ni wafanyakazi wa vituo hivyo vya afya.

Dkt Nsanzimana alisema kuwa ugonjwa huo huambukizwa kwa njia ya damu na maji maji kutoka kwa watu wenye ugonjwa huo.

Pia ameongeza kuwa inaweza kuchukua hadi wiki tatu kwa aliyeambukizwa kutoonesha dalili zozote za ugonjwa huo.

“Ni ugonjwa hatari sana, kiasi kwamba yule aliyeambukizwa anaweza kupoteza uhai,” alisema.

Virusi vya Marburg vinatajwa na wataalamu wa afya kuwa sawa na virusi hatari vya Ebola, vikiwa vimegunduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1967 nchini Ujerumani baada ya watu 9 kuambukizwa na saba kufariki dunia.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Kombe la Dunia: Mchezaji wa Ghana Thomas Partey azuiwa kuingia Canada
Mashambulizi ya Ukraine yanaathiri uchumi wa Urusi, lakini pia “unaimarika kwa haraka”: Putin
Mauritania yawaokoa wahamiaji 500 ndani ya siku 10 huku wengi zaidi wakijaribu kuvuka
Misri yatoa wito kwa Marekani, Iran 'kwa fursa' ya makubaliano baada ya Trump kusitisha mashambulizi
Ronaldo na Messi Kombe la Dunia mara ya 6
"Makubaliano makubwa" yamefikiwa na Iran: Trump
Bajeti ya trilioni 62.33 Tanzania na kupanda kwa gharama ya maisha
Raia 262 wa Nigeria wanaokimbia mashambulizi dhidi ya wageni Afrika Kusini warudishwa nyumbani
Vikosi vya Marekani na Nigeria vyawakata makali zaidi ya magaidi 200 kaskazini mashariki
Mabadiliko ya uchumi Nigeria, Uganda na nchi nyengine za Afrika yamekuza uwekezaji: Benki Kuu
Serikali ya Somalia yasikitishwa na hatua ya kuzuiwa kwa mwamuzi wa nchi hio kuingia Marekani
Watu wasiopungua 12 wauawa katika mashambulizi ya risasi jijini Johannesburg
Refa wa Somalia arudi nyumbani baada ya kukataliwa kuingia Marekani
Trump: Helikopta ya Jeshi la Marekani imedunguliwa na Iran, tutalipiza kisasi
Wakazi wa Afrika Kusini KwaZulu-Natal katika tahadhari baada ya simba kutoroka hifadhi ya wanyama
FIFA yamuondoa mwamuzi kutoka somalia Artan katika Kombe la Dunia baada ya kuzuiwa kuingia Marekani
Waandamanaji wanaopinga kujengwa kwa kituo cha Marekani cha Ebola wakamatwa nchini Kenya
Mwendesha Mashtala wa ICC asimamishwa kazi kwa madai ya dhulma za ngono
Mahakama Kuu ya Kenya: Mchakato wa kumuondoa Gachagua madarakani ulifuata Sheria
Mwamuzi wa kwanza wa Somalia aliyetarajiwa kuchezesha  Kombe la Dunia azuiwa kuingia Marekani