| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki miongoni mwa mataifa yaliyo katika makubaliano ya kulinda bahari
Mkataba wa kulinda bahari katika maeneo ya kimataifa ni mwanzo mpya unaoweka utaratibu wa kuratibu shughuli za baharini, ikiwemo marufuku ya uvuvi, katika maeneo yaliyotengwa kama hifadhi.
Uturuki miongoni mwa mataifa yaliyo katika makubaliano ya kulinda bahari
Bayram Ozturk, mkuu wa Taasisi ya Uturuki ya Utafiti wa Baharini (TUDAV), alieleza makubaliano kuwa mwanzo mpya katika kulinda bahari duniani. /AA
16 Januari 2026

Mkataba wa kulinda bahari, unaojulikana kama makubaliano ya BBNJ, utaanza kutekelezwa Jumamosi tarehe 17, baada ya kuidhinishwa na mataifa 60, kuashiria hatua muhimu ya kulinda viumbe katika bahari za kimataifa.

Makubaliano hayo ambayo yalipitishwa na Umoja wa Mataifa 2023, yanaweka utaratibu wa kisheria ya kuwa na maeneo yanayolindwa baharini na kuhitaji kufanyike tathmini ya mazingira kwa shughuli za baharini ambazo huenda zikaleta madhara kwa viumbe kwenye maji.

Uturuki ni sehemu ya makubaliano

Kote duniani maeneo 16,600 ya baharini yanayolindwa ni asilimia 9.6 ya bahari ulimwenguni, lakini asilimia 3.2 ndiyo yanayolindwa kikamilifu, ikiwa ni pamoja na kuratibu shughuli za uvuvi, hii ni kulingana na Taasisi ya Kulinda maeneo ya Bahari ya Marine Protection Atlas.

Akizungumza na Anadolu, Bayram Ozturk, mkuu wa Taasisi ya Uturuki kuhusu Utafiti wa Baharini (TUDAV), alieleza makubaliano hayo kuwa mwanzo mpya katika kulinda bahari duniani.

Alisisitiza kuwa maeneo yanayolindwa baharini hayapigi marufuku kote katika bahari ya kimataifa, lakini inatengeneza utaratibu wa kuratibu shughuli, ikiwemo kupiga marufuku katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya hifadhi.

Utekelezaji kikamilifu wa makubaliano ya BBNJ kutasaidia kulinda viumbe vya baharini na kuleta usawa katika kuratibu masuala ya bahari, alisema.

Levent Bilgili wa Kitivo cha Mafunzo ya Bahari katika Chuo Kikuu cha Bursa anasema mkataba huo utahitaji meli za mataifa yanayoshiriki katika kulinda na kufanya operesheni kwenye bahari za kimataifa kutimiza viwango vya hali ya juu na kulinda mazingira.

Kongamano la Umoja wa Mataifa la Tabianchi (COP31), lililopangwa kufanyika mwezi Novemba, linatarajiwa kufanyika mjini Antalya, katika pwani ya Uturuki ya Mediterani, huku mkutano wa viongozi ukitarajiwa kufanyika jijini Istanbul.

Kama moja ya mataifa yaliyo kwenye makubaliano ya BBNJ, kushiriki kwa Uturuki kikamilifu kunaimarisha nafasi yake kama wenyeji wa COP31, ambapo masuala yanayohusiana na bahari na tabianchi yanatarajiwa kuwa kwenye agenda, Bilgili ameiambia Anadolu.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Rais wa Uturuki awasili Ethiopia kwa ziara rasmi
Emine Erdogan awatuza wasukuma mabadiliko wakati wa makala ya 7 ya tuzo za TRT World
Rais wa Uturuki aelekea Ethiopia kwa ziara ya kikazi
Waziri Mkuu wa Somalia apongeza uchimbaji mafuta wa 'kihistoria' baharini na Uturuki
Uturuki inapanua utaalam wa reli, kutoa mafunzo kwa wafanyakazi Afrika, Asia
Erdogan: Uturuki inaendelea kutafuta amani ya kanda licha hofu iliyopo ulimwenguni
Rais wa Uturuki ateuwa Waziri mpya wa Katiba na Mambo ya Ndani katika mabadiliko ya Baraza la Mawazi
Fidan wa Uturuki akataa mashambulizi ya anga kama njia ya kubadilisha uongozi wa Iran
Makamu wa Rais wa Uturuki akutana na balozi wa Brazil
Idadi ya watu nchini Uturuki yafikia milioni 86 kwa mwaka 2025
Uturuki yalaani shambulizi la RSF nchini Sudan
Matetemeko ya ardhi ya Uturuki 2023 yalisababisha hasara ya dola bilioni 250: Erdogan
Fidan wa Uturuki akutana na Kamishna wa Maswala ya Wanachama wa EU, kujadili masuala ya ushirikiano
Rais wa Uturuki aadhimisha kumbukumbu ya miaka 3 ya tetemeko la ardhi
Uturuki imelaani shambulizi la kigaidi nchini Nigeria lililoua takriban watu 170
Uturuki kuimarisha uwepo wake wa kijeshi kuisaidia Somalia kupambana na ugaidi
Uturuki na Saudi Arabia kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na uwekezaji katika ndege za kivita za KAAN
Mke wa Rais wa Uturuki amekutana na mwenzake wa Misri jijini Cairo
Erdogan na Sisi waimarisha ushirikiano kati ya Uturuki na Misri wajadili Gaza na migogoro ya kikanda
Kikao cha mwisho cha Jukwaa la Biashara kati ya Uturuki na Misri chafunguliwa jijini Cairo