Wanajeshi wawili wa Afrika Kusini wameanguka katika mgodi wakati wa operesheni ya kukabiliana na uchimbaji madini haramu, msemaji wa polisi amesema.
Vifo hivyo ni vya kwanza kutokea tangu Rais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini kupeleka wanajeshi mwezi Machi kusaidia operesheni ya polisi dhidi ya uchimbaji madini haramu.
Tukio hilo limetokea siku ya Ijumaa katika mgodi uliotelekezwa magharibi mwa Johannesburg ambapo wanajeshi walikuwa wanawafuatilia wachimba migodi haramu, wanaojulikana kama "zama zama," amesema msemaji wa polisi Athlenda Mathe.
Wanajeshi walianguka katika mgodi uliotelekezwa, amesema.
‘Wanajeshi wenye ujasiri'
Jeshi la Ulinzi la Taifa la Afrika Kusini (SANDF) limesema tukio hilo limetokea saa kumi na mbili alfajiri.
Limesema jitihada zinaendelea za kuwatambua rasmi wanajeshi hao na kuzijulisha familia zao.
"Ni pigo kubwa kwa ulinzi na kwa taifa kwa ujumla kupoteza wanajeshi hawa," amesema kaimu Waziri wa Polisi Firoz Cachalia.
Wengi wa wachimbaji haramu ni raia kutoka mataifa jirani.













