Israel inaweza kuiangazia Uturuki kama adui baada ya Iran: Mwanadiplomasia mwandamizi wa Uturuki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki ameeleza wasiwasi kuhusu mkakati wa kanda wa Israel, akitoa wito wa kuwepo kwa makubaliano ya usalama Mashariki ya Kati, na kuonya kuhusu hatari Syria na Lebanon huku hali ya taharuki ikiendelea.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan anasema Israel inaweza kuhamisha mtazamo wa kimkakati kuangazia Uturuki kama adui katika kanda baada ya Iran, akionya kuwa sera ya Israel inategemea zaidi katika kutafuta maadui nje ya nchi.
Akizungumza na shirika la Anadolu siku ya Jumatatu, Fidan anasema Israel “inalenga kuiangazia Uturuki kama adui mwingine baada ya Iran,” akiongeza kuwa “haiwezi kujiendeleza bila kuwa na adui,” akieleza tathmini ya Uturuki kuhusu mtazamo wa Israel katika kanda.
Fidan alitoa wito kwa nchi za Mashariki ya Kati kuunda mfumo rasmi wa usalama wa kikanda kwa misingi ya kuheshimu uhuru, mipaka ya taifa, na usalama wa nchi, akieleza kuwa makubaliano kama hayo ni muhimu kuimarisha uhusiano wa muda mrefu katika kanda.
‘Lebanon inakumbusha Gaza’
Amesema Israel inafanya mashambulizi ya kijeshi nchini Lebanon yanayofanana na mashambulizi ya Gaza, akieleza uharibifu mkubwa wa nyumba na miundombinu kama sehemu ya kile alichokieleza kuwa “harakati za kuondoa watu katika sehemu zao.”
Kuhusu Syria, Fidan ameonya kuwa mashambulizi ya Israel huko yamesababisha “matatizo makubwa” na ni “hatari sana” kwa Uturuki, akiongeza kuwa kujizuia kwa sasa kwa Israel ni kutokana na kuwa wanaangazia mzozo wa Iran lakini huenda hali hiyo isiwepo kwa muda mrefu.
Kuhusu mpango mpana wa diplomasia, alisema Iran na Marekani wanaonekana kuwa “wakweli” katika kuendeleza mchakato wa kusitisha mapigano lakini akaonya watu wengine wanaweza kuchochea mchakato huo.
Fidan pia alisisitiza kuhusu msaada wa Uturuki wa kufunguliwa kwa Mlango Bahari wa Hormuz kwa njia ya amani, akionya kuwa mashambulizi ya kijeshi yatasababisha hatari zaidi, huku akisisitiza umuhimu wa ulimwengu kuhakikisha kuwa meli zinapita bila tatizo.
Akiangazia shirika la NATO, alieleza kuhusu mkutano unaotarajiwa jijini Ankara Julai 7–8, 2026, huenda ukawa na umuhimu zaidi katika historia ya shirika hilo na fursa ya kuimarisha uhusiano zaidi kati ya NATO na Marekani.