| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
DRC yaripoti maambukizi zaidi ya 6,000 ya Ebola yaliyothibitishwa
Tangu mlipuko huo kutangazwa mwezi Mei, maambukizi ya Bundibugyo yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 2,900 nchini DRC, kulingana na mamlaka za afya.
DRC yaripoti maambukizi zaidi ya 6,000 ya Ebola yaliyothibitishwa
Mlipuko mashariki mwa Congo unasambaa kutokana na watu kuondoka katika makazi yao, mgomo wa wahudumu wa afya na watu kuhamahama.

Maambukizi yaliyothibitishwa ya Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yamepita zaidi 6,000 siku ya Jumatau huku mamlaka zikiongeza juhudi za kukabiliana na mlipuko huo, takwimu rasmi zinaonesha.

DRC imeripoti maambukizi 6,041, ikiwemo vifo 2,911, tangu mlipuko huo ulipotangazwa katikati mwa mwezi Mei, kulingana na Wizara ya Afya kuhusu hali ilivyo sasa.

Watu wasiopungua 1,366 wamepona, ilhali wagonjwa 619 wametengwa au wako hospitali.

Mlipuko wa sasa wa Ebola nchini DRC ni wa pili kwa ukubwa duniani kwa maambukizi yaliyorekodiwa, kulingana na Shirika la Afya Duniani (WHO).

Maambukizi

Mlipuko huo, uliosababishwa na virusi vya Bundibugyo, yameathiri maeneo 60 ya afya katika mikoa sita: Haut-Uele, Ituri, Kivu Kaskazini, Kivu Kusini, Bas-Uele na Tshopo.

Juhudi za wizara hiyo zimeendeleza kuimarishwa katika maeneo yenye maambukizi mengi, huku mkoa wa Ituri ukiangaziwa zaidi, kutokana na kuwepo kwa maambukizi mengi na maeneo ya afya yaliyoathirika.

Kuongezeka kwa maambukizi katika kipindi cha miezi mitatu iliopita kumetajwa kuwa “kiwango kikubwa” kwa maambukizi, kulingana na WHO.

Serikali imeanzisha chanjo ya Ebola ikilenga zaidi wahudumu wa afya.

CHANZO:TRT Afrika and agencies