| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Mahakama ya ICC yampata na hatia kiongozi wa kwanza wa wapiganaji Darfur
Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman, ambaye pia anajulikana kwa jina la Ali Kushayb, anakabiliwa na makosa 31 ya uhalifu ikiwa ni pamoja na ubakaji, mauaji na mateso yanayodaiwa kutekelezwa huko Darfur kati ya Agosti 2003 na Aprili 2004.
Mahakama ya ICC yampata na hatia kiongozi wa kwanza wa wapiganaji Darfur
Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman, aliyejulikana pia Ali Kushayb amepatikana na hatia kwa mashitaka 27
6 Oktoba 2025

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu Jumatatu ilimtia hatiani kiongozi wa kwanza wa wapiganaji kuwahi kufikishwa mahakamani kwa ukatili alioufanya katika jimbo la Darfur nchini Sudan zaidi ya miaka 20 iliyopita.

Mahakama imempata Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman na hatia ya makosa 27 ya uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na ubakaji, mauaji na mateso.

Hukumu yake itatolewa baadaye baada ya hatua nyingine kusikilizwa.

Hukumu katika kesi ya kwanza na ya pekee inayohusu uhalifu nchini Sudan tangu kesi hiyo kupelekwa mahakamani na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mwaka 2005 ni ishara ya kihistoria kwa ICC.

Bado kuna hati za kukamatwa kwa maafisa wa Sudan, ikiwa ni pamoja na mmoja anayemtuhumu Rais wa zamani Omar al-Bashir kwa mashtaka ya mauaji ya halaiki.

Kukamatwa kwake

Ali Muhammad Ali Abd-Al-Rahman, ambaye pia anajulikana na nom de guerre Ali Kushayb, anakabiliwa na makosa 31 ya uhalifu ikiwa ni pamoja na ubakaji, mauaji na mateso yanayodaiwa kutekelezwa huko Darfur kati ya Agosti 2003 na angalau Aprili 2004.

Waendesha mashtaka wanasema alikuwa kiongozi wa wapiganaji maarufu wa Sudan wa Janjaweed, ambao walishiriki "kwa nguvu" katika uhalifu wa kivita.

Lakini Abd-Al-Rahman, ambaye alizaliwa mwaka 1949 amekana mashtaka yote akiiambia mahakama kwamba wamepata mtu ambaye siye wanaemtafuta.

"Mimi sio Ali Kushayb. Simjui mtu huyo... sina uhusiano wowote na mashtaka dhidi yangu," aliiambia mahakama katika kikao cha Disemba 2024.

Abd-Al-Rahman alikimbilia Jamhuri ya Afrika ya Kati Februari 2020 wakati serikali mpya ya Sudan ilipotangaza nia yake ya kushirikiana na uchunguzi wa ICC.

Alisema baada ya hapo alijisalimisha kwa sababu alikuwa "amekata tamaa" na alihofia viongozi wangemuua.

"Nilikuwa nikisubiri kwa muda wa miezi miwili nikiwa mafichoni, nikizunguka kila sehemu, na nilionywa kuwa serikali inataka kunikamata, na niliogopa kukamatwa," alisema.

Mapigano yalizuka katika jimbo la Darfur nchini Sudan wakati makabila yasiyo ya Kiarabu, yakilalamikia ubaguzi wa kimfumo, yalichukua silaha dhidi ya serikali inayotawaliwa na Waarabu.

Khartoum ilijibu kwa kuwaachilia Janjaweed, kikosi kilichotolewa kutoka miongoni mwa makabila ya kuhamahama ya eneo hilo.

Umoja wa Mataifa unasema watu 300,000 waliuawa na milioni 2.5 walikimbia makazi yao katika mzozo wa Darfur kwenye miaka ya 2000.

Soma zaidi
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32