| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi Madagascar asema ‘anachukua nafasi ya urais’
Ofisi ya Rais aliyeondolwa madarakani wa Madagascar imelaani “hatua haramu” iliyotolewa na kikosi cha kijeshi kuhusu kusimamishwa kutumika kwa katiba.
Kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi Madagascar asema ‘anachukua nafasi ya urais’
Kikosi CAPSAT, kilitangaza Jumanne kwamba kimesimamisha kutumika kwa katiba. /
15 Oktoba 2025

Kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi Madagascar amesema kupitia shirika la habari la Associated Press akiwa kambini kwake Jumatano kwamba “anachukua nafasi ya urais.”

Kanali Michael Randrianirina, aliyeongoza uasi wa wanajeshi alimuondoa mamlakani Rais Andry Rajoelina, alisema anatarajia kuapishwa kuwa kiongozi mpya wa taifa hilo la Bahari ya Hindi katika siku chache zijazo.

Vile vile alisema anachukua wadhifa wa mkuu wa nchi baada ya Mahakama ya Katiba ya Juu ya nchi hiyo kumwalika kufanya hivyo, kufuatia kutoweka kwa Rajoelina, ambaye alikimbia Madagascar baada ya uasi huo.

Mapema Jumanne, ofisi ya Rais aliyeondolewa Madagascar ililaani kile ilichokiita “hatua haramu” iliyolotolewa na kikosi maalum cha kijeshi cha CAPSAT kuhusu kusitishwa kutumika kwa katiba.

Mapinduzi ya kijeshi

Ofisi ya Rais iliita kikosi cha CAPSAT kama “kundi la waasi wa kijeshi”, na kuongeza ya kwamba uwepo wa jeshi katika ikulu ya rais ni “kitendo cha wazi cha jaribio la mapinduzi na ukiukaji mkubwa wa sheria za Jamhuri.”

“Tendo hilo ni uvunjaji wa wazi wa Katiba, misingi ya demokrasia, na kiapo cha kila mwanajeshi cha kulinda Taifa na taasisi zake halali,” taarifa hiyo ilisema.

Kikosi cha maalum cha kijeshi cha CAPSAT, kilitangaza Jumanne kwamba kimesimamisha kutumika kwa katiba na kumuondoa Rais Andry Rajoelina madarakani kwa kuzingatia hoja ya bunge ya kumwondoa madarakani, pamoja na kuchukua mamlaka, kulingana na mwandishi wa Anadolu.

CHANZO:TRT World and Agencies
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti