| swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi Madagascar asema ‘anachukua nafasi ya urais’
Ofisi ya Rais aliyeondolwa madarakani wa Madagascar imelaani “hatua haramu” iliyotolewa na kikosi cha kijeshi kuhusu kusimamishwa kutumika kwa katiba.
Kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi Madagascar asema ‘anachukua nafasi ya urais’
Kikosi CAPSAT, kilitangaza Jumanne kwamba kimesimamisha kutumika kwa katiba. /
15 Oktoba 2025

Kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi Madagascar amesema kupitia shirika la habari la Associated Press akiwa kambini kwake Jumatano kwamba “anachukua nafasi ya urais.”

Kanali Michael Randrianirina, aliyeongoza uasi wa wanajeshi alimuondoa mamlakani Rais Andry Rajoelina, alisema anatarajia kuapishwa kuwa kiongozi mpya wa taifa hilo la Bahari ya Hindi katika siku chache zijazo.

Vile vile alisema anachukua wadhifa wa mkuu wa nchi baada ya Mahakama ya Katiba ya Juu ya nchi hiyo kumwalika kufanya hivyo, kufuatia kutoweka kwa Rajoelina, ambaye alikimbia Madagascar baada ya uasi huo.

Mapema Jumanne, ofisi ya Rais aliyeondolewa Madagascar ililaani kile ilichokiita “hatua haramu” iliyolotolewa na kikosi maalum cha kijeshi cha CAPSAT kuhusu kusitishwa kutumika kwa katiba.

Mapinduzi ya kijeshi

Ofisi ya Rais iliita kikosi cha CAPSAT kama “kundi la waasi wa kijeshi”, na kuongeza ya kwamba uwepo wa jeshi katika ikulu ya rais ni “kitendo cha wazi cha jaribio la mapinduzi na ukiukaji mkubwa wa sheria za Jamhuri.”

“Tendo hilo ni uvunjaji wa wazi wa Katiba, misingi ya demokrasia, na kiapo cha kila mwanajeshi cha kulinda Taifa na taasisi zake halali,” taarifa hiyo ilisema.

Kikosi cha maalum cha kijeshi cha CAPSAT, kilitangaza Jumanne kwamba kimesimamisha kutumika kwa katiba na kumuondoa Rais Andry Rajoelina madarakani kwa kuzingatia hoja ya bunge ya kumwondoa madarakani, pamoja na kuchukua mamlaka, kulingana na mwandishi wa Anadolu.

CHANZO:TRT World and Agencies
Soma zaidi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi
Majeshi ya Somalia yawaua viongozi watatu wakuu wa Al Shabaab
Rwanda, DRC zaanzisha mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi huku kukiwa na mazungumzo ya amani
RSF yazika miili katika makaburi ya halaiki, inachoma wengine ili 'kuficha ushahidi wa mauaji
Wananchi katika Al Fasher, Sudan, wanakabiliwa na ukatili 'wa kiwango kisichoweza kuaminika' — UN
Chama tawala nchini Djibouti kimemteua Rais Guelleh kwa muhula wa sita
Amaan Golugwa akamatwa huku polisi Tanzania ikiwasaka viongozi wa upinzani kufuatia maandamano
Wafanyakazi waokolewa baada ya maharamia kushambulia meli ya mafuta kutoka Somalia