| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Rais Erdogan amejadili uhusiano wa pande mbili, masuala ya kimataifa na Rais Rodriguez wa Venezuela
Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amesema kuwa nchi yake itaendelea kuimarisha ushirikiano na Venezuela katika maeneo mbalimbali, hasa biashara, nishati na madini.
Rais Erdogan amejadili uhusiano wa pande mbili, masuala ya kimataifa na Rais Rodriguez wa Venezuela
Pande hizo mbili pia zilijadili hatua za kufikia lengo la biashara la Dola bilioni 3. / / AA

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na kaimu Rais wa Venezuela Delcy Rodriguez walijadili uhusiano wa nchi mbili na maendeleo ya kimataifa wakati wa mazungumzo huko Istanbul, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Uturuki imesema.

Katika taarifa ya Jumatatu iliyowekwa kwenye mtandao wa kijamii wa Uturuki NSosyal, kurugenzi hiyo ilisema Erdogan alikutana na Rodriguez na wajumbe wake, ambao wanafanya ziara ya kikazi Uturuki.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Idara ya Mawasiliano ya Uturuki, Erdogan alisema kwamba Uturuki itaendelea kuwa pamoja na watu rafiki wa Venezuela.

Pia alisisitiza kuwa Uturuki imejipanga kuendeleza zaidi ushirikiano na Venezuela katika sekta mbalimbali, hususan biashara, nishati na uchimbaji madini.

Viongozi hao wawili pia walijadili hatua za kufikia lengo la kuongeza biashara ya pande mbili kufikia Dola bilioni 3.

Kabla ya mazungumzo hayo, Erdogan alimpokea Rodríguez kwa hafla rasmi katika Ikulu ya Rais ya Dolmabahçe.

Baada ya mapokezi hayo, viongozi hao walifanya mazungumzo ya faragha ya pamoja na wajumbe wao.

Rodríguez alitembelea Uturuki kwa mwaliko wa Rais Erdogan.

Katika mazungumzo hayo pia walihudhuria viongozi mbalimbali wa Uturuki, wakiwemo Makamu wa Rais, Cevdet Yilmaz, Waziri wa Mambo ya Nje, Hakan Fidan, Waziri wa Nishati, Alparslan Bayraktar, Waziri wa Viwanda na Teknolojia Mehmet Fatih Kacir, Waziri wa Biashara, Omer Bolat, Mkurugenzi wa Mawasiliano Burhanettin Duran, na Akif Cagatay Kilic, Mshauri wa sera za nje na usalama.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Rais Erdogan: Mkutano wa NATO ulikuwa wa mafanikio makubwa
Trump ampongeza Rais Erdogan, akiuita mkutano wa NATO kuwa wa mafanikio
Uturuki yatafuta uhusiano wa kibiashara na uwekezaji zaidi na washirika wa NATO
Vikwazo vya CAATSA ni nini na kuondolewa kwake na Marekani kutainufaishaje Uturuki?
Rais Erdogan wa Uturuki aimarisha ahadi yake kwa NATO kupitia ufadili katika ulinzi
Viongozi wa NATO wafungua siku ya mwisho ya mkutano wa Ankara wakilenga Arctic, Iran, na Ukrain
Uhusiano wa usalama kati ya Afrika na Uturuki unazidi kuimarika katika mfumo wa dunia unaobadilika
Rais Erdogan wa Uturuki awaandalia mchapalo viongozi wa NATO na wenzi wao
Uturuki yalenga kushirikiana na washirika wa NATO
Uturuki yazindua 'limousine' maalum za Togg kwa viongozi wanaohudhuria mkutano wa kilele wa NATO
Ripoti: Trump yuko tayari kurejesha uwezo wa Uturuki kupata ndege za F-35
Usalama wa Ulaya hauwezi kufungiwa ndani ya EU, asema Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Fidan
Viongozi wa NATO waanza kukusanyika mjini Ankara kwa mkutano wa kilele wenye mada muhimu
Uturuki ipo tayari kiusalama kuelekea mkutano wa NATO
Uturuki yaandaa kituo maalumu cha habari kwa ajili ya mkutano wa NATO
Ulaya itatumia mkutano wa NATO mjini Ankara kumwonyesha Trump uthabiti wake katika ulinzi
Rais Erdogan wa Uturuki aonya dhidi ya Israel iliyozoea vita, kuhujumu makubaliano ya amani ya Iran
Rais wa Uturuki Erdogan amempokea Waziri Mkuu wa Pakistan Sharif mjini Istanbul
Kwa nini juhudi za Uturuki za kudumisha uwiano ni muhimu kwa NATO
Jinsi mfumo wa Uturuki wa upatanishi na ushirikiano wa ulinzi unavyoimarisha usalama barani Afrika