Siku tatu za maombolezo Ethiopia kufuatia maporomoko ya ardhi
Maporomoko ya ardhi yamegharimu maisha ya takriban watu 80 katika Jimbo la Kusini mwa Jimbo la Ethiopia.
Ethiopia imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa baada ya maporomoko ya ardhi katika eneo la Gamo, Jimbo la Kusini mwa Ethiopia.
Maporomoko hayo ya ardhi yameua watu wasiopungua 80.
Siku za mvua kubwa zilisababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi, huku maji yakiongezeka kutoka Mto Kulfo uliotitirika katika vitongoji na kuharibu nyumba, mashamba na miundombinu ya ndani.
Waziri Mkuu Abiy Ahmed alitembelea eneo hilo Jumamosi, punde tu baada ya kuwasili nchini kutoka UAE ambako alikwenda kikazi.
"Serikali itaendelea kutoa msaada unaohitajika kwa wananchi wenzetu walioathirika,"
aliwaambia watu katika eneo hilo lililoathiriwa na maporomoko.
"Tafiti lazima pia zifanyike ili kutatua tatizo kwa njia endelevu. Hatua za kuzuia pia ni muhimu," aliongezea.
Serikali ya Ethiopia inasema shughuli za kutafuta miili iliyosalia zinaendelea.
Huku kipindi cha maombolezo cha siku tatu kinaanza bendera ya taifa la Ethiopia zitapeperushwa nusu mlingoti nchini, kwenye meli za Ethiopia na katika balozi zote za Ethiopia nje ya nchi.