| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Siku tatu za maombolezo Ethiopia kufuatia maporomoko ya ardhi
Maporomoko ya ardhi yamegharimu maisha ya takriban watu 80 katika Jimbo la Kusini mwa Jimbo la Ethiopia.
Siku tatu za maombolezo Ethiopia kufuatia maporomoko ya ardhi
Maporomoko ya ardhi yauwa zaidi ya watu 80 katika jimbo la Kusini la Ethiopia / picha: @AbiyAhmedAli / Public domain
14 Machi 2026

Ethiopia imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa baada ya maporomoko ya ardhi katika eneo la Gamo, Jimbo la Kusini mwa Ethiopia.

Maporomoko hayo ya ardhi yameua watu wasiopungua 80.

Siku za mvua kubwa zilisababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi, huku maji yakiongezeka kutoka Mto Kulfo uliotitirika katika vitongoji na kuharibu nyumba, mashamba na miundombinu ya ndani.

Waziri Mkuu Abiy Ahmed alitembelea eneo hilo Jumamosi, punde tu baada ya kuwasili nchini kutoka UAE ambako alikwenda kikazi.

"Serikali itaendelea kutoa msaada unaohitajika kwa wananchi wenzetu walioathirika,"
aliwaambia watu katika eneo hilo lililoathiriwa na maporomoko.

"Tafiti lazima pia zifanyike ili kutatua tatizo kwa njia endelevu. Hatua za kuzuia pia ni muhimu," aliongezea.

Serikali ya Ethiopia inasema shughuli za kutafuta miili iliyosalia zinaendelea.

Huku kipindi cha maombolezo cha siku tatu kinaanza bendera ya taifa la Ethiopia zitapeperushwa nusu mlingoti nchini, kwenye meli za Ethiopia na katika balozi zote za Ethiopia nje ya nchi.

Soma zaidi
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Somalia yashtumu uteuzi wa balozi wa Israel katika eneo lililojitenga la Somaliland
Uganda inasema inahitaji zaidi ya Dola bilioni moja kusambaza umeme nchini kote
Afrika Kusini yampa kifungo cha miaka mitano jela Julius Malema kwa kufyatua risasi
DRC inaanzisha hifadhi ya kimkakati ya kobalti na madini mengine
Afrika Kusini yamkamata mwanaharakati wa Benin Kemi Seba kwa tuhuma za uchochezi
Burkina Faso yafuta takriban asasi 100 za kiraia
Rais wa Cameroon anasema dunia inahitaji 'ujumbe wa amani' wa Papa
Jeshi la Tanzania latangaza nafasi ajira
Raia wa China ahukumiwa jela kwa kusafrisha mchwa kutoka Kenya kinyume cha sheria
Iran yatishia kuzuia usafiri wa meli katika Bahari ya Shamu ikiwa vikwazo vya Marekani vitaendelea
Marie-Louise Eta: Mwanamama aliyepewa mikoba Bundesliga
Mamia wajitokeza Afrika Kusini kabla ya hukumu ya kifungo cha mwanasiasa Malema
Wasichana ndio waathirika wakubwa zaidi katika vita vilivyosahaulika vya Sudan
Bei ya mafuta yapanda Kenya huku usambazaji ukisuasua