Urusi imesema kuwa ipo tayari kuisaidia serikali ya Msumbiji kupambana na vitisho vya kigaidi nchini humo.
Uamuzi huo, unafuatia ombi lilitoka kwa Rais Daniel Francisco Chapo, mara baada ya kukutana na Waziri wa Mambo wa Nje wa Urusi, Sergey Lavrov.
"Kati ya mambo mengine ambayo tumejadiliana, ni mapambano dhidi ya ugaidi," alisema Lavrov.
ZILIZOPENDEKEZWA
"Urusi ipo tayari kuwasaidia marafiki zetu wa Msumbiji kutokomeza tatizo la ugaidi nchini Msumbiji."
Lavrov aliwasili jijini Maputo siku ya Alhamisi, baada ya kuzitembela Ethiopia na Niger.
CHANZO:reuters












