Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amesema pendekezo jipya la sheria linalolenga kuimarisha mshikamano wa kitaifa na umoja wa kijamii ni hatua muhimu katika juhudi za Uturuki za kuondoa kabisa tishio la ugaidi.
“Baada ya mashauriano ya kina, Muswada wa Kuimarisha Mshikamano wa Kitaifa na Umoja wa Kijamii uliwasilishwa leo mbele ya Bunge Kuu la Kitaifa la Uturuki kwa kuungwa mkono kwa mapana, jambo linaloonyesha azma ya taifa letu pendwa ya kufikia suluhisho la kudumu,” Erdogan alisema katika ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii Jumatano baada ya muswada huo kuwasilishwa bungeni.
“Ninatumaini kwamba hatua hii, ambayo inalenga kuiondoa kabisa Uturuki kutoka kwenye tishio la ugaidi, kuimarisha umoja na mshikamano wetu wa kitaifa, pamoja na kuimarisha hali ya amani na utulivu nchini mwetu na katika eneo lote, italeta matokeo chanya,” aliongeza Erdogan.
Erdogan pia alivishukuru vyama vya siasa, makundi ya vyama vya siasa bungeni na wabunge walioshiriki katika mchakato wa kuandaa na kukamilisha pendekezo hilo la sheria.




















