Nigeria: Watu 7 wauawa katika mashambulizi ya silaha na wengine 32 watekwa nyara
Watu saba waliuawa na wengine 32 walitekwa nyara wakati wa mashambulizi yaliyofanyika katika jimbo la Niger, Magharibi mwa Nigeria.
Nigeria School Kidnappings / Photo: AP / AP
Kulingana na vyombo vya habari vya eneo hilo, watu wasiojulikana wenye silaha walishambulia vituo vya polisi katika mikoa ya Kontagora na Mashegu kwenye Jimbo la Niger, na kuua watu saba, wakiwepo polisi wawili.
Viongozi wamenalaani idadi kubwa ya majeraha na utekaji nyara wa watu 32. Ingawa uhalifu wa utekaji nyara unaadhibiwa kwa kifo inchini Nigeria, utekaji nyara kwa fidia huwa unajitokeza mara kwa mara.
Kwa kupambana na vitisho vya utekaji nyara vinavyoongezeka huko Nigeria, malipo ya fidia kwa watu wenye silaha yamepigwa marufuku na serekali.