Rwanda yapiga hatua katika uzalishaji wa nishati ya nyuklia

Kulingana na Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), Rwanda imepiga hatua kubwa katika kuongeza nguvu za nyuklia katika nishati zake.

By
Rais Paul Kagame wa Rwanda./Picha:@PaulKagame

Rwanda imepiga hatua katika kuongeza nguvu ya nyuklia katika orodha ya nishati zake, Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) limesema.

Taarifa hiyo inafuatia tathmini ya hivi karibuni iliyofanywa hivi karibuni na timu ya wataalamu kutoka shirika hilo.

Rwanda inalenga kusambaza kati ya asilimia 60 hadi 70 ya nishati yake kutoka nguvu za nyuklia.

Kulingana na shirika la IAEA, hatua kubwa imepigwa na taifa hilo, hususani katika kutengeneza kanuni na sheria za nishati hiyo.