| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Kampuni ya ulinzi ya Uturuki yapata kandarasi ya mamilioni ya dola kulinda mipaka ya nchi moja Afrika.
Kampuni ya Asisguard, yenye makao yake katika mji mkuu wa Uturuki Ankara, imetia saini mkataba wa dola milioni 36.5, ikijumuisha ndege zisizo na rubani, uchunguzi na mifumo ya kamera za utambuzi/ugunduzi.
Kampuni ya ulinzi ya Uturuki yapata kandarasi ya mamilioni ya dola kulinda mipaka ya nchi moja Afrika.
Mradi unajumuisha bidhaa za utambuzi/ugunduzi, amri na udhibiti, na madhumuni ya tahadhari. Picha: AA / Others
28 Mei 2023

Kampuni ya ulinzi ya Uturuki imetia saini mkataba wa mamilioni ya dola na nchi ya Kiafrika ili kusambaza mahitaji yake ya mpaka na usalama wa ndani.

Asisguard, ambayo inafanya kazi katika nyanja za ndege zisizo na rubani, macho ya kielektroniki, na uboreshaji wa magari, ilitia saini mkataba wa takriban dola milioni 36.5 na nchi hiyo, kulingana na data iliyopatikana na Anadolu. Jina la nchi halijatolewa.

Mradi unajumuisha bidhaa za utambuzi/ugunduzi, amri na udhibiti, na madhumuni ya tahadhari/uingiliaji kati.

Kwa mradi huo, kampuni ya Uturuki, yenye makao yake makuu katika mji mkuu Ankara, itafanya shughuli za usanikishaji na ujumuishaji wa mfumo kwa kutumia ndege zisizo na rubani zenye silaha, uchunguzi na mifumo ya kamera za utambuzi/ugunduzi.

Makampuni ya Kituruki Havelsan, STM, na Nurol Makina pia wanahusika katika mradi huo, ambao ni mfano wa kazi ya pamoja ya ng'ambo na shughuli za uuzaji kwa tasnia ya ulinzi ya Uturuki.

Mshikamano wa makampuni hayo uliripotiwa kuwa mojawapo ya vipengele muhimu katika kushinda kandarasi.

CHANZO:AA