Kwa picha : Siku ya tatu ya mashindano ya kimataifa ya magari nchini Kenya
Serikali inasema hafla hiyo ya World Rally Championship inavutia zaidi ya wageni 100,000, na kuunda nafasi za kazi zenye thamani ya zaidi ya dola milioni 175.
mashindano ya magari ya safari rally yameingia siku ya tatu nchini Kenya (WRC) msimu wa 2023 / Picha: AFP / AFP
Mashindano hayo yamevutia timu 34 kutoka nchi 20
Mji wa Naivasha ndiyo kivutio kikuu nchini Kenya hasa kwa mashabiki wa magari .
Mashabiki wamebuni njia ya kuona magari ambayo yanapita mbali
Mashindano hayo yamevutia mashabiki kutoka nchi zingine pia kama nchi jirani ya Uganda
Kwa wale ambao lazima wafanye kazi lazima wavumilie wingu zito la vumbi linalozuka wakati magari yanapopita kwa mbio
Mashabiki wengine walitafuta maeneo ya starehe ili kutazama shindano hilo
Madereva nao wanajimudu ili kutoa msisimko ambao mashindano haya yanahusika nayo