| swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Bunge la Ghana laidhinisha kuondolewa hukumu ya kifo
Ghana iko inaelekea kuwa nchi ya 29 kukomesha hukumu ya kifo barani Afrika na ya 124 duniani kote.
Bunge la Ghana laidhinisha kuondolewa hukumu ya kifo
Ghana inajiunga namataifa mengine 123 yaliyofuta hukumu y akifo duniani Picha : Getty
26 Julai 2023

Bunge la Ghana limepiga kura kufuta hukumu ya kifo, na kuifanya nchi hiyo kuwa ya hivi punde kati ya mataifa kadhaa ya Afrika ambayo yamechukua hatua ya kufuta adhabu ya kifo katika miaka ya hivi karibuni.

Hakuna mtu aliyenyongwa nchini Ghana tangu 1993, ingawa watu 176 walikuwa kwenye orodha ya kunyongwa kufikia mwaka jana, kulingana na huduma ya magereza ya Ghana.

Mswada huo mpya utarekebisha sheria ya makosa ya jinai ya jimbo ili kuchukua nafasi ya kifungo cha maisha jela kwa hukumu ya kifo, kulingana na ripoti ya kamati ya bunge.

Kura ya bunge ilifanyika Jumanne. Rais Nana Akufo-Addo bado anasubiriwa kuidhinisha sheria hiyo kabla kuanza kutekelezwa. Katika siku za nyuma, Rais Akufo-Addo alitoa hadharani uungaji mkono wake kwa kukomesha hukumu ya kifo.

"Hii ni hatua kubwa ya rekodi ya haki za binadamu ya Ghana," alisema Francis-Xavier Sosu, mbunge ambaye aliwasilisha mswada huo.

"Tumefanya utafiti, kuanzia marejeo ya katiba hadi kura za maoni, na zote zinaonyesha kwamba wananchi wengi wa Ghana wanataka hukumu ya kifo iondolewe," aliambia shirika la habari la Reuters.

Ghana ni nchi ya 29 kukomesha hukumu ya kifo barani Afrika na ya 124 duniani kote, kulingana na The Death Penalty Project, NGO yenye makao yake makuu London ambayo ilisema ilifanya kazi pamoja na washirika nchini Ghana kusaidia kubadilisha sheria.

Equitorial Guinea, Sierra Leone, Jamhuri ya Afrika ya Kati na Zambia ni miongoni mwa mataifa ya hivi punde barani Afrika kuondoa adhabu ya kifo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti