| Swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Hamas haipaswi kuondoka kisiasa: Balozi wa Bodi ya Amani
Nickolay Mladenov anasema kundi la upinzani la Palestina la Hamas linaweza kubaki kama kundi la kisiasa, lakini makundi yenye silaha lazima yaweke silaha chini.
Hamas haipaswi kuondoka kisiasa: Balozi wa Bodi ya Amani
Nickolay Mladenov akizungumza na waandishi wa habari Jerusalem Mashariki inayokaliwa kwa mabavu, Jumatano, Mei 13, 2026. / AP

Nickolay Mladenov amesema kundi la Palestina la Hamas linaweza kubaki kisiasa, lakini makundi yenye silaha sharti yaweke silaha chini kutokana na makubaliano ya usitishaji wa mapigano wa Gaza.

Nickolay Mladenov, mjumbe maalumu wa Bodi ya Amani anayesimamia usitishaji wa mapigano Gaza, amesema kwamba Bodi hiyo haitaki kuipoteza Hamas 'kisiasa.'

Akizungumza Jumatano katika mkutano Jerusalam Mashariki iliyokaliwa kwa mabavu, Mladenov amesema “hatutaki Hamas ipotee kama kundi la kisiasa.”

Lakini amerudia madai ya kutaka Hamas na makundi mengine kuweka silaha chini, akilielezea suala hilo kwamba "halina mjadala."

Miezi saba baada ya makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyoanza Oktoba 2025, "mlango wa mustakbali wa Gaza bado umefungwa," amesema.

“Sicho walichoahidiwa Wapalestina na sicho wanachostahiki. Na haiwapi Israel ulinzi wa kusogea mbele, kama wanavyotaka Waisrael," amesema Mladenov.

“Tunausitishaji wa mapigano. Unafanya kazi. Haujakamilika. Kuna ukiukwaji kila siku, na baadhi ni ukiukwaji mkubwa," amesema, akimaanisha ukiukwaji unaoendelea kufanywa na Israel.

Jitihada za Trump za amani

Bodi ya Amani imeundwa Januari kwa jitihada za Rais wa Marekani Donald Trump kama sehemu ya kufikia makubaliano ya amani Gaza.

Marekani baadae ilisema nchi nyengine zilijiunga katika jitihada hiyo.

Tangu kusitishwa kwa mapigano Oktoba 10, 2025, mashambulizi ya Israel yameuwa takriban Wapalestina 856 na kujeruhi 2,463, kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Gaza.

Makubaliano ya kusitisha mapigano yalifanyika baada ya miaka miwili ya mauaji ya halaiki Gaza yaliyoanza Oktoba 2023.

Mashambulizi ya Israel baadae yaliendelea katika mfumo tofauti, na kuuwa zaidi ya Wapalestina 72,000, kuwajeruhi zaidi ya 172,000 na kuharibu takriban asilimia 90 ya miundombinu ya raia Gaza.

Soma zaidi
Iran yasema makombora yako tayari huku vitisho vya Israel dhidi ya Beirut vikiongezeka
Raia wa Australia akamatwa kwa kufuga mende zaidi ya laki moja
Kiongozi wa upinzani Guinea Bissau awekwa kifungo cha nyumbani
Waafrika waliokuwa India kwa matibabu, miongoni mwa 21 waliofariki katika ajali ya moto hotelini
Iran yashambulia uwanja wa ndege wa Kuwait
Iran yashambulia kambi ya kijeshi ya Marekani nchini Kuwait, 7 wajeruhiwa
Uingereza kuzindua chombo cha AI kugundua wahamiaji watu wazima wanaodai kuwa watoto
Serikali ya Trump inataka noti ya $250 inayoonesha picha yake: ripoti inasema
Syria yagundua mkusanyiko wa silaha za kemikali kutoka mpango wa zamani wa serikali ya Assad
Tumeshambulia kambi ya jeshi la Marekani nchini Kuwait: Vikosi vya Iran (IRGC)
Waislamu waswali swala ya Eid al-Adha katika Msikiti wa Al-Aqsa
Takriban Waislamu milioni 2 wanatarajiwa kutekeleza ibada ya Hajj huku mahujaji wakielekea Mina
Israel inahofia kuwa Trump atafuata makubaliano yenye mipaka ya Iran, na kuacha mpango wa nyuklia
'Wamepata vidonda mwilini' — wanaharakati wasimulia mateso waliyopitia walipotekwa na Israel
Mojtaba Khamenei amesema madini ya urani ya Iran yatabaki nchini humo
Marco Rubio: Tutahakikisha Ebola haifiki Marekani
Wanaharakati wa msafara wa Flotilla walioshambuliwa na Israel wapelekwa Uturuki
Trump na Netanyahu watofautiana kwa njia ya simu kuhusu kuishambulia Iran — Ripoti
Marekani na Israel zilipanga kumuweka madarakani rais wa zamani wa nchi hiyo Ahmadinejad
Urusi na China zaimarisha ushirikiano kwa kusaini mikataba 20 ikiwemo ya uchumi, nishati na biashara