| Swahili
AFRIKA
4 DK KUSOMA
DRC : Daktari Denis Mukwege, mshindi wa tuzo ya Nobel ya amani 2018 kugombea Urais
Daktari huyo aliyepata umaarufu kwa kuwatibu kinamama hadi kubatizwa jina la 'Baba anayewatengeneza Kinamama'
DRC : Daktari Denis Mukwege, mshindi wa tuzo ya Nobel ya amani 2018 kugombea Urais
Wagombea wengine wanayo nafasi ya kufikisha faili zao kwenye Tume ya Uchaguzi CENI kabla ya tarehe 8 mwezi huu wa Octoba ili kushiriki uchaguzi mkuu/ Picha Reuters  / Others

Na Ramadhan Kibuga

TRT Afrika, Kinshasa, DRC

Daktari Denis Mukwege, mshindi wa Tuzo ya Nobel 2018 ametangaza jumatatu hii mjini Kinshassa kwamba atakuwa mgombea wa uchaguzi wa Urais baadae tarehe 20 Disemba mwaka huu.

Daktari Denis Mukwege alitangaza uamzi huo kwenye mkutano na vyombo vya habari mjini Kinshasa.

Ameamua kuingia kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi wa rais katika hatua za mwisho kabisa na kuwasilisha faili zake kwenye Tume huru ya Kitaifa ya Uchaguzi (CENI).

''Siwezi kusubiria hadi mwaka wa 2028, Sijachukua uamuzi huu kwa sababu ya maslahi au kwa sababu ya kutaka madaraka. Lakini kwa lengo la kuokoa taifa langu. Kesho itakuwa nimechelewa. Nakwenda sasa kujitupa kwenye uchaguzi.'' Alisema Dkt Mukwege.

Uamzi huo wa Dkt. Mukwege hata hivyo ulikuwa unasubiriwa kwa miezi kadhaa. Jina lake lilikuwa linazungumzwa sana miongoni mwa watu wanaoweza kuwa wagombea wa uchaguzi. Na wiki za hivi karibuni hali iliashiria hivyo.

Watu ambao walikuwa wanasititiza wakimtaka awe mgombea wanaamini kwamba huu ndio wakati muafaka na uamzi sahihi.

''Inabidi kuwa na moyo wa kuachana na matakwa au raha za kibinafsi na kufikiria kwanza uzalendo,'' aliongeza Dkt Mukwege.

Dkt Mukwege pia alizindua azimio lake ambalo limetungwa kwa nguzo kumi na mbili, ikiwemo amani, usalama na ulinzi sambamba na kupambana dhidi ya hisia za ubaguzi nchini, na haki na sheria sawa kwa wote pamoja na utawala wa sheria.

Azimio lake linaonekana kwenda sambamba na vita ambavyo Dk Mukwege amekuwa anapigania kwa muda mrefu na hasa kutokana na kutowajibikia viongozi walioko madhila wanayopata raia.

Alianza hotuba yake akiomba ukimya wa dakika moja ili kuwakumbuka waathirika wote wa migogoro nchini DR Congo. '' Mimi ni mwananchi ambae nimehuzunishwa saana, mimi ni mwanamageuzi''. Alitangaza Bwana Mukwege '' Hatuko pamoja na raia, tumejiweka kwenye ubinafsi.''

Aidha Bwana Mukwege alikemea vikali '' Wimbi za ahadi hewa zilizofanywa na watawala wasiowajibika. Na hii imenifanya kuchukua maamuzi.''

Oroodha ya wagombea Urais

Daktari huyo aliyepata umaarufu kwa kuwatibu kinamama hadi kubatizwa jina la 'Baba anayetengeneza Kinamama'

''Nchi yangu iko hatarini. Hali ni tete Mashariki mwa Nchi yetu kukiwa na vikosi vya kigeni, Rasli mali zetu zinaporwa , dhiki ya maisha ni kubwa kwa raia, ndio maana nimeamua mara hii kugombea urais ili kumaliza changamoto hizo,'' alisema Dkt Mukwege.

Dk Mukwege anakuja kuongeza orodha ya watetezi kwenye uchaguzi huo wa urais.

Mwishoni mwa juma , Rais Felix Tchisekedi alitangaza kuwa atawania tena urais na kuongoza Muungano mkubwa wa Vyama vilivyo karibu na Serikali'' Union Sacree''.

Wakati huo huo Mpinzani Mkuu Martin Fayulu naye pia alibainisha uamzi wake wa kushiriki kwenye uchaguzi huo.

Wagombea wengine wanayo nafasi ya kufikisha faili zao kwenye Tume ya Uchaguzi CENI kabla ya tarehe 8 mwezi huu wa Octoba ili kushiriki uchaguzi mkuu ambao unatarajiwa kufanyika tarehe 20 Disemba 2023.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Mswada mpya Sudan Kusini kumpa Salva Kiir mamlaka yote ya kuwafuta kazi Makamu wake kabla uchaguzi
Sudan Kusini inasonga mbele na mipango ya mradi wa Bwawa la Grand Fula kwenye mto White Nile
Marekani inatuma dola milioni 2.5 nchini Gambia kutokana na mauzo ya kasri la rais wa zamani
Afrika Kusini yatoa zawadi ya $24,600 kwa taarifa kuhusu muuaji wa wanawake
TikTok kukata kodi kwenye mapato ya waandaaji maudhui Kenya
Mkuu wa polisi Kenya apatikana na hatia ya kudharau mahakama kufuatia maandamano ya Gen Z
Afrika Kusini yawasaka wauaji wa mtangazaji wa michezo Owen Ndlovu
Ajali ya mgodi wa dhahabu Sudan yasababisha vifo vya takriban watu 60
Mvutano wa kidiplomasia wa Marekani na Afrika Kusini waibuka tena kutokana na vikwazo vya viza
Kaka mkubwa wa mfalme mpya wa Tooro, afariki
Bunge la Libya laidhinisha kwa pamoja mpango wa uchaguzi mkuu
Jeshi la Sudan laangusha 'droni za adui' ambazo hazijatambuliwa jimbo la Kassala
Rais wa Cape Verde kugombea kwa muhula wa pili
Kwa nini Uganda wanatakiwa kutafakari kuhusu mpango wao wa kupeleka vikosi Gaza
Dawa za kulevya zenye picha ya Gaddafi zakamatwa Libya
Mataifa matano Afrika yakabiliana na milipuko ya polio, lakini mapambano bado yanaendelea
Aliyekuwa afisa wa ujasusi Uganda arejeshwa Marekani kukabiliwa na mashtaka ya magendo
Mlipuko wa ugonjwa wa kimeta waua viboko 46 na tembo wanane nchini Zambia
Mwenge wa Olimpiki wawasili Senegal kwa ajili ya Olimpiki barani Afrika
Putin anaunga mkono juhudi za Afrika za kutaka mageuzi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa