Iran imewanyonga watu wawili kwa kuhusika na shirika la kijasusi la Israel la Mossad.
Watu hao walikutwa na hatia na kufanya mazoezi , ikiwemo kuiba mawasiliano ili kuwawezesha kuandaa vilipuzi, shirika la habari la Iran (IRIB) limesema.
ZILIZOPENDEKEZWA
Pia, wanadaiwa kuwasha mioto kwenye maeneo ya kijeshi na kutuma picha mjongeo za matukio hayo ili walipwe fedha.
Hukumu hiyo inakuja wakati ambapo mamia ya raia wa Iran wakiwa kizuizini kwa madai ya “kushirikiana na maadui” toka kuanza kwa vita vya Marekani-Israel dhidi ya Iran, ambavyo vimegharimu maisha ya watu zaidi ya 3,300 hadi sasa.
CHANZO:AA


















