UTURUKI
2 dk kusoma
Rais Erdogan aifanyia majaribio gari mpya aina ya Togg T10F jijini Istanbul
Rais wa Uturuki ameendesha gari aina ya Togg sedan huku mauzo ya gari zinazotumia umeme yakiimarika na kuweka nchi hiyo katika nafasi nzuri miongoni mwa mataifa ya bara Ulaya.
Rais Erdogan aifanyia majaribio gari mpya aina ya Togg T10F jijini Istanbul
Kuimarika kwa soko la magari ya EV ni muhimu kwa agenda ya mazingira ya Uturuki, huku Togg ikiongoza katika hilo. / AA
7 Julai 2025

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan aliendesha kwa majaribio gari jipya lililozinduliwa la T10F sedan na watengenezaji wa taifa wa magari yanayotumia umeme ya Togg siku ya Jumamosi, kuashiria umuhimu wa Uturuki unaoimarika duniani katika kutengeneza magari yanayotumia umeme.

Rais Erdogan alikuwa ameongozana na Rais wa masuala ya Biashara na Viwanda wa Uturuki (TOBB) Rifat Hisarciklioglu, Mwenyekiti wa shirika la Anadolu Tuncay Ozilhan, Mwenyekiti wa shirika la Zorlu Ahmet Nazif Zorlu, Mwenyeiti wa kampuni ya Turkcell Senol Kazanci, na Mwenyekiti Shirika la Tosyali Fuat Tosyali.

Haya yanajiri wakati ambao Uturuki inapanda chati katika soko la utengenezaji magari ya umeme duniani.

‘Mafanikio makubwa’

Hivi karibuni, Uturuki imekuwa soko la nane duniani kwa mauzo ya magari ya umeme 2024, hasa kutokana na uzalishaji wa ndani ya nchi, kuwa na maeneo mengi ya ‘kuchaji’ umeme, na serikali kusaidia, kulingana na shirika la kufanya utafiti wa magari lenye makao yake Uingereza la New AutoMotive.

Mwaka uliopita, Uturuki ilifanya mauzo ya magari hayo ya EV 123,982. Mwezi Aprili 2025 pekee, nchi hiyo ilikuwa nafasi ya saba duniani, huku wakiuza magari 11,173 — zaidi ya Norway na Italia na kuwa soko linaloongoza la EV katika mataifa ya Mediterania. Disemba 2024 Uturuki ilikuwa na mauzo makubwa zaidi ya EV, ikiuza magari 17,894, na kuwa katika nafasi ya sita duniani mwezi huo.

Shirika la New AutoMotive limeeleza ukuaji wa Uturuki kama ‘‘mafanikio makubwa,” likibaini kuwa soko la magari yanayotumia betri za umeme limeimarika kwa zaidi ya asilimia 10 katika kipindi cha miezi minane mfululizo.

Kuimarika kwa soko la magari yanayotumia umeme Uturuki kunaonekana kama nguzo muhimu ya agenda yake ya kuhifadhi mazingira, huku gari aina ya Togg ikiwa na nafasi muhimu ya kubadilisha mtazamo wa mustakabali wa sekta ya utengenezaji magari.

CHANZO:trt global
Soma zaidi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan
Mfumo wa ulimwengu wa sasa unazingatia nguvu zaidi ya haki: Mkurugenzi wa TRT
Israel imeigeuza Gaza kuwa vifusi, inawezaji kuwa haina hatia: Erdogan
Uturuki yakashifu unafiki wa nchi za Magharibi kuhusu Gaza, yatoa wito wa mfumo mpya wa dunia
Hamas haina nuyklia, Israel iko nayo: Erdogan aitaka Berlin ichukue hatua kali dhidi ya Tel Aviv
Erdogan ataka kuona mabadiliko katika uhusiano na EU na ushirikiano wa kikanda alipokutana na Mertz
Ujerumani yatoa wito wa kuunda “ushirikiano wa kimkakati” ili kukabiliana na changamoto za kimataifa
"Marekebisho ya Ulimwengu": Jukwaa la 9 la TRT World kuanza Istanbul likiangazia majadiliano na haki
Erdogan ametangaza washindi wa Tuzo Kuu za Utamaduni na Sanaa za Urais mwaka 2025
Uturuki yaadhimisha miaka 102 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri
Uturuki yatoa wito wa kusitishwa mara moja kwa mapigano katika mji wa Al Fasher, Sudan
Uturuki na Jordan zasaini makubaliano ya kuimarisha uhusiano wa kiuchumi
Erdogan atangaza kukabidhiwa kwa jeshi vifaru vya kwanza  vya Altay vilivyotengenezwa Uturuki
Israel inaishutumu 'Uturuki chini ya utawala wa Erdogan’ kuwa na uhasama mkali dhidi yake
Erdogan na Starmer wasaini mkataba wa ndege za kivita za Eurofighter Typhoon
Erdogan, amkaribisha Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer, katika Ikulu ya Ankara