| swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Kiongozi wa 'ibada ya njaa' nchini Kenya apatikana na hatia ya kupiga picha haramu
Mhubiri Paul Mackenzie, amekuwa chini ya ulinzi wa polisi kwa zaidi ya miezi sita kufuatia kupatikana kwa mamia ya miili katika makaburi ya halaiki.
Kiongozi wa 'ibada ya njaa' nchini Kenya apatikana na hatia ya kupiga picha haramu
Mhubiri huyo amekuwa akizuiliwa na polisi kwa zaidi ya miezi sita sasa / Picha: Reuters
11 Novemba 2023

Paul Mackenzie, mhubiri tata wa ibada ya njaa nchini Kenya ambayo ilisababisha vifo vya zaidi ya watu 400, siku ya Ijumaa alipatikana na hatia ya kuendesha studio na kusambaza filamu bila leseni.

Hakimu mkazi mkuu katika mji wa Malindi, Olga Onalo, alimkuta Mackenzie na hatia ya kuonyesha filamu kupitia televisheni yake ya 'Times' bila idhini ya Bodi ya Kuainisha Filamu nchini Kenya.

Mhubiri huyo amekuwa akizuiliwa na polisi kwa zaidi ya miezi sita sasa tangu alipokamatwa mwezi wa Aprili, kufuatia kupatikana kwa mamia ya miili katika makaburi ya halaiki katika eneo lenye msitu katika eneo lake la ekari 800 katika kaunti ya pwani ya Kilifi.

Waendesha mashtaka wanasema Mackenzie aliamuru waumini wake kufa kwa njaa ili kukutana na Yesu.

Bado mashtaka

Hata hivyo, hajafunguliwa mashtaka rasmi kuhusu vifo hivyo, licha ya kufikishwa mahakamani mara kadhaa tangu akamatwe.

Siku ya Ijumaa alifutiwa mashtaka ya ziada ya kushawishi watoto kutohudhuria shule na kutumia mahubiri makali kuwachochea Wakristo dhidi ya Wahindu, Wabudha na Waislamu.

Atahukumiwa kwa makosa yanayohusiana na filamu mnamo Desemba 1 na anaweza kufungwa jela miaka mitano.

Siku ya Alhamisi, waendesha mashtaka waliomba Mackenzie azuiliwe kwa miezi sita zaidi ili kuruhusu polisi kukamilisha uchunguzi wao ambao ni pamoja na kutafuta makumi ya watu ambao bado hawajapatikana.

Tangu kukamatwa kwake, kumekuwa na wito kwa serikali kudhibiti makanisa nchini Kenya.

➤ Fuatilia TRT Afrika Swahili kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti