| swahili
UTURUKI
2 DK KUSOMA
Uturuki yapuuza 'madai yasiyokuwa na msingi' ya Netanyahu dhidi ya Rais Erdogan
Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu na Waziri Cohen, "ambao wote hawafurahii ukweli unaoonyeshwa, hawataweza kuficha uhalifu wao wenyewe kwa kashfa zao zisizo na msingi," Wizara ya Mambo ya Nje inasema
Uturuki yapuuza 'madai yasiyokuwa na msingi' ya Netanyahu dhidi ya Rais Erdogan
Uturuki yapuuza 'madai yasiyokuwa na msingi' ya Netanyahu dhidi ya Rais Erdogan. / Picha: AA
16 Novemba 2023

Serikali ya Uturuki imepinga "uchongezi usio na msingi " uliofanywa na waziri mkuu wa Israeli dhidi ya Rais Recep Tayyip Erdogan, huku ikisema maafisa wa Israeli" hawana haki ya kuzungumza juu ya sheria."

"Maafisa wa Israeli, ambao wameingia katika kurasa za giza za historia na ukandamizaji na mauaji yaliyofanywa dhidi ya Wapalestina, hawana haki ya kuzungumza juu ya sheria," Wizara ya Mambo ya Nje ilisema katika taarifa iliyotumwa Jumatano.

Benjamin Netanyahu "(Waziri Mkuu wa Israeli) na Eli Cohen (Waziri wa Mambo ya Nje), ambao wote hawana furaha na ukweli unaoonyeshwa, hawataweza kuficha uhalifu wao wenyewe na kashfa zao zisizo na msingi kwa Recep Tayyip Erdogan, rais wa Jamhuri ya Uturuki," iliongeza.

Wachochezi na wahusika wa uhalifu dhidi ya binadamu, uliosababisha chuki kubwa miongoni mwa mawazo ya umma duniani, hivi karibuni au baadaye watahukumiwa, Wizara ilisisitiza.

"Utawala wa Israeli, ambao tayari umepoteza uhalali wake katika dhamiri ya binadamu, hawataweza kuficha uhalifu walioufanya kwa kulipua hospitali na kuua wanawake na watoto mbele ya ulimwengu wote na hawataweza kugeuza umakini," ilisema.

Uturuki itaendelea kusimama dhidi ya mauaji huko Gaza, Palestina na kuunga mkono haki za watu wa Palestina, Wizara imeongeza.

CHANZO:TRT World
Soma zaidi
Fidan: Njia ya kusuluhisha vikwazo vya Marekani iko wazi huku Trump akionyesha nia yake
Rais Erdogan aadhimisha kumbukumbu ya miaka 42 ya kuanzishwa kwa TRNC
Rais Erdogan afungua maonyesho ya 'Echoes' Istanbul kwa heshima ya Sule Yuksel Senler na Malcolm X
Uturuki yaadhimisha miaka 81 ya kupelekwa uhamishoni Waturuki wa Ahiska kutoka Georgia
Hafla yafanyika Uturuki ya kuwakumbuka wanajeshi waliofariki kwenye ajali ya ndege
Wanajeshi 20 wa Uturuki wafariki katika ajali ya ndege ya mizigo ya kijeshi huko Georgia: wizara
Wanajeshi 20 wa Uturuki wauawa katika ajali ya ndege ya shehena ya kijeshi huko Georgia: wizara
Ndege ya kijeshi ya mizigo ya Uturuki yaanguka mpakani mwa Georgia na Azerbaijan ikiwa na watu 20
Uimarishaji wa Uturuki ni heshima na kumuenzi Ataturk: Erdogan
Uturuki inamkumbuka Ataturk miaka 87 baada ya kufariki
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki kuzuru Marekani siku ya Jumatatu
Rais Erdogan anatumai Marekani itatimiza ahadi zake kuhusu makubaliano ya ndege za kivita za F-35
Palestina inapongeza amri za kukamatwa dhidi ya maafisa 37 wa Israel kutoka Uturuki kama 'ushindi
Ujumbe wa Erdogan 'Azerbaijan haiko peke yake' ulipelekea ushindi wa Karabakh: Aliyev
Ushindi wa Karabakh wa Azerbaijan kwa amani ya Caucasus: Rais Erdogan
Uturuki yatoa hati ya kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Netanyahu, juu ya mashtaka ya mauaji
Erdogan: Uturuki kuharakisha miradi ya kiulinzi kuimarisha ‘maslahi’ na washirika wa Ulaya
Uturuki kuandaa mazungumzo ya Gaza wiki ijayo kufuatia wasiwasi juu ya usitishaji mapigano – Fidan
Mfumo wa ulimwengu wa sasa unazingatia nguvu zaidi ya haki: Mkurugenzi wa TRT
Israel imeigeuza Gaza kuwa vifusi, inawezaji kuwa haina hatia: Erdogan