Sam Allison: Muamuzi wa kwanza mweusi kweny Premier League tangu 2008
Refa Sam Allison kuweka historia ligi kuu ya mpira Uingereza kwa kuwa mwamuzi mweusi wa kwanza Premier League tangu 2008.
Refa Sam Allison anatarajiwa kuweka historia kwenye ligi kuu ya Uingereza baadaye leo kwenye mechi kati ya Sheffield United na Luton Town kwa kuwa mwamuzi wa kwanza mweusi kusimamia mechi kwenye Ligi kuu hiyo tangu 2008.
Hata hivyo, sio mara ya kwanza kuwa katika baadhi ya marefa mechini, kwani mnamo mwezi Oktoba 2022, alikuwa refa wa nne katika mechi kati ya Brighton & Hove Albion na Chelsea.
Sam Allison atasaidiwa na: James Mainwaring, na Nick Greenhalgh, mkuu wa mechi: Andy Madley, refa wa VAR: Michael Salisbury na aibu wa VAR: Derek Eaton.
Mwamuzi wa mwisho mweusi kushikilia kipenga mechini alikuwa Uriah Rennie, ambaye alihudumu katika ligi hiyo kwa zaidi ya miaka 10 hadi kufikia 2008.
Ingawa kwa sasa ni refa, Sam Allison aliwahi kuwa mchezaji na alikipiga Swindon Town, Bristol City, AFC Bournemouth na Exeter City kabla ya kustaafu.
Tangu alipopandishwa daraja na kuwa muamuzi wa viwango vya juu mnamo 2020, Allison amekuwa mwamuzi wa tano mweusi kuongoza mechi katika ligi ya daraja la pili EFL, akifuata nyayo za Rennie, Trevor Parkes, Phil Prosser na Joe Ross.