| swahili
AFRIKA
3 DK KUSOMA
Uturuki haitaacha kufichua uongo wa Israeli: Mkurugenzi wa Mawasiliano Altun
Akisisitiza kujitolea kwa uwajibikaji wa dunia yenye haki, Fahrettin Altun amesema kwamba, jitihada kama uanzishwaji wa tuzo ya TRT World Citizen unahusisha jitihada kabambe za kupitiliza katika vyombo vya habari ili kufikia mustakbali mzuri zaidi.
Uturuki haitaacha kufichua uongo wa Israeli: Mkurugenzi wa Mawasiliano Altun
Altun amesisitiza jitihada za Israeli za kueneza propaganda yenye giza kupitia maafisa, wasomi, na vyombo vya habari. Amehakikisha, "Mara hii, hawatafanikiwa." / Picha: AA
20 Januari 2024

Israeli inatengeza propaganda yake ya giza kutokana na uongo na inajaribu kueneza kupitia maafisa, wasomi, na vyombo vya habari, amesema Mkurugenzi wa Mawasiliano Fahrettin Altun.

"Katu hatutakata tamaa kwa kufichua upotoshaji wa Israeli na kudhihirisha ukweli katika ajenda ya dunia," amesema mkurugenzi.

Katika hotuba yake kwenye sherehe ya tuzo za TRT World Citizen Ijumaa, Altun amesema watu wenye fikra za kikoloni wanawatesa wale wenye fikra tofauti na wao. Amesisita, "Maonevu ya sasa ya Israeli dhidi ya Palestina, ni kiashiria cha fikra za kikoloni, ambayo inadhihirisha wazi matendo hayo."

Altun amesema mfumo wa sasa wa kimataifa, ambao umeanguka katika uso wa udhalilishaji wa Gaza, unaonyesha ni kwa nini kuna lazima ya kufanyika mabadiliko, na kusema, "Mashirika mengi ya utangazaji ya nchi za magharibi yanaonyesha kuunga mkono Israeli, kugemea upande mmoja, na kubadilisha ukweli."

"Katika mashambulizi ambayo yamekuwa yakiendelea kwa zaidi ya siku 100, Israeli inafanya propaganda za giza na upotoshaji kupitia vyombo vya habari vya kimataifa na makampuni ya mitandao ya kijamii."

Kutokana na uwajibikaji wa kibinadamu, Uturuki katu haibadiliki katika mashambulizi hayo, inasimama pamoja na watu wa Palestina wanaodhulumiwa, na itaendelea kufanya hivyo, amesema.

Altun amedokeza kwamba, mradi wa tuzo za Citizen Awards kupitia TRT ni jitihada za kila mmoja kuonyesha uwezo wake wa kuleta mabadiliko chanya.

'Israeli haitafanikiwa katika propaganda yake ya giza'

Amesema, mapambano makubwa ya kibinadamu dhidi ya mauaji ya Israeli yameonyeshwa na waandishi wa habari wanaofanya kazi katika eneo hilo, Altun amesema kwamba waandishi wa habari "sio tu wametoa taarifa lakini pia wamepigana katika mapambano matakatifu ya kuonyesha ukweli, na waandishi 119 wa Palestina wamekufa mashahidi katika jitihada hizo."

Juhudu zisizokuwa za kawaida za waandishi waliopo Gaza zimepelekea kuwepo kwa wimbi chanya la mabadiliko duniani kote, amesema.

"Sababu kwa nini Israeli imekuwa ikilenga kwa makusudi waandishi wa habari ni kwa sababu ya ukweli na msimamo wa haki wa waandishi ...Dunia nzima inajua kwamba Israeli kwa makusudi imelenga waandishi wa habari kama vile Wael al Dahdouh anaetafuta ukweli, kwa makusudi imeua familia yake." Ameongeza kwamba, Israeli inajaribu kuuwa ukweli na kuuziba pumzi."

"Haki pekee yake haitoshi, ni lazima kuwa bora zaidi. Tutapambana katika siasa, diplomasia, msaada wa kibinadamu, mawasiliano, na vyombo vya habari, kumaliza janga hili," ameongeza.

CHANZO:TRT World
Soma zaidi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi
Majeshi ya Somalia yawaua viongozi watatu wakuu wa Al Shabaab
Rwanda, DRC zaanzisha mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi huku kukiwa na mazungumzo ya amani
RSF yazika miili katika makaburi ya halaiki, inachoma wengine ili 'kuficha ushahidi wa mauaji
Wananchi katika Al Fasher, Sudan, wanakabiliwa na ukatili 'wa kiwango kisichoweza kuaminika' — UN
Chama tawala nchini Djibouti kimemteua Rais Guelleh kwa muhula wa sita
Amaan Golugwa akamatwa huku polisi Tanzania ikiwasaka viongozi wa upinzani kufuatia maandamano
Wafanyakazi waokolewa baada ya maharamia kushambulia meli ya mafuta kutoka Somalia