| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Kenya yasitisha mpango wa kupeleka polisi Haiti
Kenya imetangaza kusitisha mpango wake wa kupeleka maafisa wa polisi nchini Haiti kufuatia kujiuzulu kwa Waziri Mkuu wa Haiti Ariel Henry
Kenya yasitisha mpango wa kupeleka polisi Haiti
Magenge na majangili wamewazidi wananchi nchini Haiti / Photo: AFP / AFP
12 Machi 2024

Kenya imeamua kusitisha mipango ya kutuma polisi kwenda Haiti, iliyoathiriwa na vurugu, chini ya ujumbe wa kimataifa unaoungwa mkono na UN, afisa mkuu wa wizara ya mambo ya nje alisema Jumanne.

Korir Sing'oei, katibu mkuu wa mambo ya nje, aliambia AFP kwamba kumekuwa na "mabadiliko ya msingi katika mazingira kama matokeo ya sheria kutokufuatwa na kujiuzulu kwa Waziri Mkuu wa Haiti (Ariel Henry)".

Maamuzi ya Sing'oei yanakuja wiki moja baada ya Henry kushuhudia utiaji saini wa ombi la kupeleka polisi ambalo Haiti ilifanya rasmi kwa Kenya. Waziri mkuu alikuwa nchini Kenya kwa ziara ya siku mbili.

Jumanne, Henry alijiuzulu baada ya siku kadhaa za machafuko nchini humo, huku muungano wenye nguvu wa magenge ukidai kuondolewa kwake, wakimlaumu kwa kudorora kwa uchumi katika taifa la Caribbean, na pia kumtuhumu kuwa ni kibaraka wa Marekani.

Baraza la mpito

Henry, ambaye ni mtaalamu wa upasuaji wa ubongo, alikanusha madai hayo.

Katika ujumbe wa video akitangaza kujiuzulu kwake, Henry alisema yeye na serikali yake wataondoka ofisini "mara moja baada ya kufungwa kwa baraza la mpito."

Henry, mwenye umri wa miaka 74, alichaguliwa kuwa waziri mkuu wa Haiti na Rais Jovenel Moise tarehe 5 Julai, 2021.

Siku mbili baadaye, Moise aliuawa katika mji mkuu wa Port-au-Prince.

Henry, baadaye, alichukua nafasi kama kiongozi wa nchi, na aliahidi kuondoka ofisini ifikapo Februari 7, 2024, lakini aliahirisha uchaguzi kwa madai ya machafuko nchini.

Pata habari zaidi kupitia whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika