| swahili
AFRIKA
3 DK KUSOMA
Sudan: Vikosi vya kijeshi 'vimeua 50 katika mashambulizi ya vijiji'
Mashambulizi dhidi ya vijiji katika jimbo la Al-Jazirah yalifuatia kuasi hivi majuzi kwa makamanda wakuu wa RSF katika eneo hilo.
Sudan: Vikosi vya kijeshi 'vimeua 50 katika mashambulizi ya vijiji'
Vikosi vya Msaada wa Dharura hivi karibuni viliidungua ndege ya mizigo ya Urusi katika eneo la Al Malha nchini Sudan. Picha / Reuters
26 Oktoba 2024

Wanaharakati wa ndani nchini Sudan siku ya Ijumaa walishutumu Vikosi vya Msaada wa Dharura (RSF) kwa kuwaua takriban raia 50 na kuwajeruhi wengine 200 wakati wa mashambulizi dhidi ya vijiji katika jimbo la Al-Jazirah, Sudan ya kati.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan hapo awali ilishutumu RSF kwa kufanya "mashambulizi ya kulipiza kisasi" katika jimbo la Al-Jazirah, lililoko kusini mwa mji mkuu, Khartoum.

Mashambulizi hayo yalifuatia kuasi hivi majuzi kwa makamanda wakuu wa RSF katika eneo hilo.

Kamati ya upinzani katika mji wa Al-Hasaheisa iliripoti kwamba kijiji cha Al-Suraih kimekuwa kikishambuliwa na vikosi vya RSF tangu Ijumaa asubuhi, na kusababisha vifo vya wakaazi 50.

Kuzingirwa

Imeongeza kuwa kijiji kingine cha jirani, Azrak, kinaendelea kuzingirwa na kinakabiliwa na mashambulizi yanayoendelea kufanywa na vikosi vya RSF.

RSF bado haijatoa maoni yoyote kuhusu madai hayo.

Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) liliripoti Ijumaa kuwa kaya 853 zilihamishwa kutoka mji wa Tamboul na vijiji jirani katika jimbo la Al-Jazirah kati ya Oktoba 20 na 24, 2024, kutokana na kuongezeka kwa mapigano kati ya jeshi la Sudan na RSF.

Matukio hayo yanakuja siku chache baada ya Abu Aqla Muhammad Ahmed Kikil, kamanda wa RSF huko Al-Jazirah, kutangaza kujitoa kwa jeshi la Sudan, na kuchukua vikosi vyake pamoja naye.

Maeneo ya mashariki mwa Al-Jazirah, eneo alikozaliwa Kikil, yamekuwa ngome ya vikosi vyake, ambavyo sasa vinapigana pamoja na jeshi.

Mnamo Desemba 2023, vikosi vya Kikil vya RSF viliteka udhibiti wa miji kadhaa huko Al-Jazirah, pamoja na mji mkuu wa jimbo, Wad Medani, ulioko kusini mwa Khartoum.

Tangu katikati ya mwezi wa Aprili 2023, jeshi la Sudan na RSF zimekuwa zikiingia kwenye mzozo mbaya, ambao umesababisha vifo vya zaidi ya 20,000 na kuwakimbia zaidi ya watu milioni 10, kulingana na UN.

Wito kutoka kwa jumuiya ya kimataifa na Umoja wa Mataifa kuhusu kukomesha ghasia umeongezeka huku mzozo huo ukitishia kuwaingiza mamilioni katika njaa kutokana na uhaba wa chakula katika majimbo 13 kati ya 18 ya Sudan.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Kiongozi wa zamani wa waasi wa DRC anayeshtakiwa Paris kwa uhalifu wa kivita aanza mgomo wa kula
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32