Tanzania: Idadi ya vifo vilivyotokana na jengo kuporomoka yafikia 29

Vifo vilivyotokana ajali hiyo vimefikia 29, baada ya miili mingine tisa kupatikana wakati zoezi la uokozi likiendelea.

By Edward Josaphat Qorro
Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Thobias Makoba akizungumza na waandishi wa habari./Picha:  @TZMsemajiMkuu / Others

Idadi ya watu waliopoteza maisha katika tukio la kuporomoka jengo nchini Tanzania, sasa imefikia 29, serikali ya nchi hiyo imesema.

Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania Thobias Makoba, amesema kuwa shughuli nzima ya uokoaji katika eneo la soko la Kariakoo, imekamilika siku ya Novemba 26, huku idadi ya vifo vinavyotokana na tukio hilo la Novemba 16 ikifikia 29.

Hii ni baada ya kupatikana kwa miili mingine tisa, wakati wa zoezi la uokozi likiendelea, serikali hiyo imesisitiza.

“Kuanzia Novemba 26, eneo lote la Kariakoo linafunguliwa huku shughuli mbalimbali zikiendelea...isipokuwa eneo moja tu lililohusisha ghorofa kuporomoka ndilo litaendelea kufungwa kwa siku tatu kwa ajili ya kumalizia zoezi la uchunguzi,” alisema Makoba.

Kwa mujibu wa Msemaji huyo, kazi ya uokoaji kwenye jengo lililoporomoka Kariakoo imehitimishwa baada ya kuokolewa kwa watu wote waliokuwa hai na waliopoteza maisha.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels