Uganda: Maporomoko ya ardhi yaua watu 30

Kulingana na mamlaka ya nchi hiyo, janga hilo pia limeharibu makazi ya watu.

By Edward Josaphat Qorro
Uganda imeshuhudia mvua kubwa katika siku za karibuni./Picha: Wengine / Others

Watu 30 wamepoteza maisha kufuatia maporomoko ya ardhi katika kijiji kimoja huko mashariki ya Uganda.

"Tumepoteza watu wapatao 30," mkuu wa wilaya ya Bulambali, Faheera Mpalanyi ameiambia AFP baada ya kijiji chake cha Masugu kukumbwa na maporomoko hayo.

Tukio hilo limetokea miezi mitatu baada ya watu kadhaa kupoteza maisha kwenye tukio kama hilo.

"Kulingana na hali ilivyo, tunahisi kuwa kuna watu kadhaa wamefunikwa kwenye udongo," alisema.

Tukio hilo limesababisha uharibu wa kaya 40.

Mvua Kubwa

Hadi sasa, miili 13 imeopolewa kufuatia shughuli za uokoaji zilizofanywa na Shirika la Msalaba Mwekundu la Uganda.

Kulingana na Waziri Mkuu wa Uganda, kuna hofu kuwa nyumba zaidi ya 20 zimefunikwa.

Pata habari zaidi kupitia whatsapp channels