| swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Wanafunzi Uganda wachelewa kumaliza shahada ya uzamili
Bunge la Uganda limepata ushahidi unaoonyesha kuwa kwa wastani, wanafunzi walichukua zaidi ya miaka minne ya masomo kukamilisha utafiti wa shahada ya uzamili ilhali muda ulioidhinishwa kwa mafunzo ya chuo kikuu ni miaka 2.
Wanafunzi Uganda wachelewa kumaliza shahada ya uzamili
Bunge la Uganda linachunguza kwa nini wanafunzi wengi hawamalizi shahada ya uzamivu katika chuo kikuu cha Makarere / Picha:  MUBS
21 Januari 2025

Chuo kikuu cha Makerere nchini Uganda kimeanza kuchunguzwa baada ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Edward Akol kugundua kuwa zaidi ya wanafunzi 400 wa Shahada ya Uzamili walishindwa kumaliza masomo yao kwa wakati uliotarajiwa.

Bunge la Uganda limepata ushahidi unaoonyesha kuwa kwa wastani, wanafunzi walichukua zaidi ya miaka minne ya masomo kukamilisha utafiti wa shahada ya uzamili ilhali muda ulioidhinishwa kwa mafunzo ya chuo kikuu ni miaka 2.

Wakati huo huo chuo kingine kinachofahamika kama Kitivo cha Biashara cha Chuo Kikuu cha Makerere pia kimewekwa kwenye uangalizi baada ya wanafunzi 322 wa Shahada ya Uzamili kugunduliwa kuwa wamechukua wastani wa zaidi ya miaka 4 ya masomo kukamilisha utafiti wa masomo hayo.

Hii ni zaidi ya muda ulioidhinishwa wa chuo kikuu kwa programu za uzamili za miaka 2.

Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Edward Akol amebainisha kuwa kati ya wanafunzi 3,044 waliojiandikisha kwa ajili ya masomo mbalimbali ya uzamili katika kipindi cha miaka kumi (mwaka wa masomo 2013/14 hadi 2020/2021), wanafunzi 1,931 walihitimu na kuacha wanafunzi 1,113 ambao bado hawajahitimu.

Zaidi ya hayo, Akol ameliambia bunge pia kati ya wanafunzi 190 waliojiandiakisha kwa Programu za Uzamivu kwa kipindi cha miaka 10 (mwaka wa masomo 2013/14 hadi 2020/2021) ni wanafunzi 60 tu ndio waliohitimu. Wanafunzi 130 bado hawajahitimu.

Amesema baadhi ya ucheleweshaji huo ulichangiwa na ucheleweshaji wa usimamizi na changamoto zinazohusiana na wanafunzi kama vile uhaba wa fedha.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi
Majeshi ya Somalia yawaua viongozi watatu wakuu wa Al Shabaab
Rwanda, DRC zaanzisha mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi huku kukiwa na mazungumzo ya amani
RSF yazika miili katika makaburi ya halaiki, inachoma wengine ili 'kuficha ushahidi wa mauaji
Wananchi katika Al Fasher, Sudan, wanakabiliwa na ukatili 'wa kiwango kisichoweza kuaminika' — UN
Chama tawala nchini Djibouti kimemteua Rais Guelleh kwa muhula wa sita
Amaan Golugwa akamatwa huku polisi Tanzania ikiwasaka viongozi wa upinzani kufuatia maandamano
Wafanyakazi waokolewa baada ya maharamia kushambulia meli ya mafuta kutoka Somalia