| Swahili
AFRIKA
3 DK KUSOMA
Ofisi ya Uhuru Kenyatta yasema juhudi zake kwa amani ya DRC hazizingatiwi
Mchakato wa Nairobi ( Nairobi Process) kama unavyofahamika ni mchakato unaoongozwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki kama mpango wa amani wa kikanda unaolenga kutatua mzozo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Ofisi ya Uhuru Kenyatta yasema juhudi zake kwa amani ya DRC hazizingatiwi
Rais mstaafu wa Kenya, Uhuru Kenyatta anaongoza Mchakato wa amani wa Nairobi waJumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuhusu amani DRC /Picha : @4thPresidentKE / Others
6 Februari 2025

Ofisi ya Rais mstaafu wa Kenya, Uhuru Kenyatta imeeleza wasiwasi kuwa juhudi za mchakato wa amani unaoongozwa na Kenyatta hazijazingatiwa katika mzozo unaoendelea nchini DRC.

" Mchakato wa amani wa Nairobi, licha ya kuwa ulisitishwa kwa muda, unasalia kuwa mchakato muhimu wa mazungumzo na utatuzi wa migogoro mashariki mwa DRC. Mratibu anaendelea kujitolea kutafuta njia za amani, kwa ushirikiano na serikali ya DRC, washirika wa kikanda, na wadau wa kimataifa," Kanze Dena msemaji wa ofisi ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta amesema.

Mchakato wa Nairobi ( Nairobi Process) kama unavyofahamika ni mchakato unaoongozwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki kama mpango wa amani wa kikanda unaolenga kutatua mzozo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Ulizinduliwa mnamo Aprili 2022, kwa msingi wa kanuni za ujumuishaji, mazungumzo, umiliki, uongozi wa kikanda na usaidizi wa kimataifa huku Uhuru Kenyatta akiwa mjumbe maalum.

Chini ya mchakato huu viongozi wa EAC ambapo DRC ni mwanachama waliamua kupeleka Jeshi la Kanda ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACRF) Mashariki mwa DRC mnamo Novemba 2022 kwa lengo la kurejesha amani na utulivu, dhidi ya kikundi chenye silaha cha M23.

Kwa sasa mchakato wa Umoja wa Afrika wa kuleta amani DRC unaoongozwa na Rais wa Angola Joao Lourenco ndiyo ambao unaonekana kupewa kipaumbele.

" Mratibu wa mchakato huu ana imani thabiti kwamba michakato miwili ya Luanda na Nairobi ina mipango mikubwa zaidi ya utatuzi na kumaliza mgogoro wa mashariki mwa DRC. Michakato hii miwili ni ya kuridhisha na inawiana." ofisi ya Rais mstaafu Kenyatta imesema.

" Ni kupitia tu uratibu wa karibu wa mazungumzo ya pande mbili kati ya Rwanda na DRC na Mchakato wa Mazungumzo na Mikutano ya Ndani ya DRC ndipo mgogoro huu unaweza kupata suluhu yenye tija," ofisi imeongeza.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Marekani yawawekea vikwazo wapiganaji wa Colombia nchini Sudan
Kundi la kwanza la waliofukuzwa kutoka Marekani lawasili Kinshasa nchini DRC
Mtoto wa Mugabe akiri kumtishia mtu kwa bunduki nchini Afrika Kusini
Nigeria yapiga marufuku kusimikwa kwa ‘Wafalme wa Igbo’ nje ya nchi
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uturuki, Misri, Pakistan, Saudia kukutana Jukwaa la Diplomasia Antalya
Somalia inasema hatua ya Israel kuunga mkono Somaliland inakiuka Uhuru wa Somalia
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Somalia yashtumu uteuzi wa balozi wa Israel katika eneo lililojitenga la Somaliland
Uganda inasema inahitaji zaidi ya Dola bilioni moja kusambaza umeme nchini kote
Afrika Kusini yampa kifungo cha miaka mitano jela Julius Malema kwa kufyatua risasi
DRC inaanzisha hifadhi ya kimkakati ya kobalti na madini mengine
Afrika Kusini yamkamata mwanaharakati wa Benin Kemi Seba kwa tuhuma za uchochezi
Burkina Faso yafuta takriban asasi 100 za kiraia
Rais wa Cameroon anasema dunia inahitaji 'ujumbe wa amani' wa Papa
Jeshi la Tanzania latangaza nafasi ajira