| Swahili
AFRIKA
2 DK KUSOMA
Waziri wa mambo ya nje wa Djibouti ndiye mkuu wa Tume ya AU
Mahmoud Ali Youssouf aliwashinda Raila Odinga wa Kenya na Richard Randriamandrato, waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Madagascar.
Waziri wa mambo ya nje wa Djibouti ndiye mkuu wa Tume ya AU
Mahmoud Ali Youssouf atahudumu kwa muhula wa miaka minne . Picha : TRT Afrika / Others
16 Februari 2025

Viongozi wa Afrika walimchagua waziri wa mambo ya nje wa Djibouti kuwa kiongozi ajaye wa tume hiyo kuliko uongozi wa Umoja wa Afrika katika bara zima.

Mahmoud Ali Youssouf amewashinda Raila Odinga, waziri mkuu wa zamani wa Kenya, na Richard Randriamandrato, waziri wa mambo ya nje wa zamani wa Madagascar, katika kura iliyopigwa kwenye mkutano wa AU mjini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia.

AU ina nchi wanachama 55. Marais au wakuu wa serikali huchagua kiongozi wa tume, ambaye ni mtendaji mkuu wa sekretarieti yenye makao yake makuu mjini Addis Ababa inayoendesha AU.

Youssouf, ambaye atahudumu kwa muhula wa miaka minne, anachukua nafasi ya Moussa Faki wa Chad, ambaye ameshikilia wadhifa huo tangu 2017.

Randriamandrato akubali kushindwa

Aliyekuwa mgombea uenyekiti wa Tume ya Afrika kutoka Madagascar Richard Radrimandrato, amekubali kupoteza nafasi hiyo kwa Mdjibouti Mahmoud Ali Youssouf katika uchaguzi uliofanyika makao makuu ya Umoja wa Afrika, jijini Addis Ababa Ethiopia

Radrimandrato, ambaye kura zake hazikutosha na kulazimika kujitoa kwenye kinyang’anyiro hicho, alikubali matokeo hayo kupitia ukurasa wake wa X.

Kwa upande wake, Raila Odinga wa Kenya pia alishindwa kupata theluthi mbili ya kura kama inavyohitajika na Umoja wa Afrika.

Pata habari zaidi kupitia Whatsapp channels

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Afrika Kusini yaomba utulivu kufuatia maandamano dhidi ya kusimikwa kwa 'Igwe' wa Nigeria
Rwanda ‘yahofia’ operesheni za DRC dhidi ya kikundi cha FDLR
Kenya yalipa ada ya Dola milioni 30 ya uenyeji wa AFCON 2027
Hasara ya mamilioni kufuatia ubomoaji katika soko kubwa zaidi la wazi la Gikomba Nairobi
Shabiki maarufu ‘Lumumba Vea’ akosa viza ya  kwenda kuishangilia DRC dhidi ya Jamaica
Mamlaka ya uchukuzi Kenya yazindua ukaguzi wa lazima wa afya kwa madereva ili kupunguza ajali
Tanzania yahimiza matumizi ya AI kuimarisha mtangamano na maendeleo EAC
Kundi lenye silaha limewaua watu wasiopungua 20 Jimbo la Plateau nchini Nigeria
Wafungwa wasiopungua 11 wafariki kutokana na mlipuko wa kipindupindu katika jela DRC
Kagame awaamuru maafisa waandamizi wa serikali 'kusimama' wakati wa hotuba yake
Wadukuzi wadukua maombi ya kazi 450,000 nchini Afrika Kusini
Rais wa Misri asema ni Trump pekee anaweza kusimamisha vita, aonya kupanda zaidi kwa bei ya mafuta
Togo yatoa uzoefu wa kupambana na magonjwa yasiyopewa kipaumbele
Watu 15 wamefariki katika ajali ya barabarani mkoa wa kati Kenya
Mahakama kuu ya Jamhuri ya Congo imethibitisha ushindi wa Sassou Nguesso kwa awamu ya tano
Rwanda, Burundi wanagombana juu ya juhudi za rais wa zamani wa Senegal Sall kuongoza UN
Vifo kutokana na mafuriko nchini Kenya vyaongezeka hadi 108, polisi wasema
Majenerali wakuu wa Uganda wazuiliwa kwa madai ya ufisadi: ripoti
Eswatini yamrudisha nyumbani mwananchi wa Cambodia aliyefukuzwa kutoka Marekani
Waasi waanza kuondoka katika vijiji vya DRC ili kuhimiza amani