| swahili
AFRIKA
3 DK KUSOMA
Mwanasiasa Besigye wa Uganda arudishwa gerezani
Kizza Besigye na msaidizi wake, Hajj Obeid Lutale, walifikishwa katika Mahakama Kuu ya Kampala kwa ajili ya kusikilizwa kwa ombi la kutaka waachiliwe
Mwanasiasa Besigye wa Uganda arudishwa gerezani
Mwanasiasa mkongwe wa upinzani nchini Uganda Dkt. Kizza Besigye na msaidizi wake Hajj Obeid Lutale wamerudishwa gerezani. / Picha  kwa hisani ya  Kampala Post.
19 Februari 2025

Mwanasiasa mkongwe wa upinzani nchini Uganda Dkt. Kizza Besigye na msaidizi wake Hajj Obeid Lutale wamerudishwa katika gereza la Luzira chini ya ulinzi mkali baada ya kusikilizwa kwa ombi lao katika Mahakama Kuu mjini Kampala.

Besigye na msaidizi wake, Hajj Obeid Lutale, walifikishwa katika Mahakama Kuu Kampala kwa ajili ya kusikilizwa kwa ombi la kutaka waachiliwe.

Kesi hiyo mbele ya Jaji Douglas Singiza, ilitokana na ombi lililowasilishwa na wanasheria wa Besigye Februari 5, la kutaka maelezo kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Kamishna Mkuu wa Magereza kuhusu kuendelea kuzuiliwa kwa mwanasiasa huyo.

Jaji Singiza alieleza wasiwasi kuhusu hali ya afya ya Besigye, akisema kwamba hangeweza kuendelea huku mgonjwa akiendelea kuwepo mahakamani.

"Ikiwa mfungwa ni mgonjwa, siwezi kuendelea na kesi. Anaweza kuzimia,” alisema jaji Singiza.

Besigye amekuwa katika mgomo wa kula huku akilalamika kucheleweshwa kwa kesi yake.

Hakimu aliamuru Besigye na Lutale warudishwe gerezani badala ya kubaki mahakamani.

Besigye na Obeid wamekuwa rumande tangu Novemba 2024 baada ya kutekwa nyara wakiwa jijini Nairobi nchini Kenya.

Baadaye walishtakiwa kwa makosa yanayohusiana na usalama na uhaini katika Mahakama Kuu ya kijeshi ya Uganda.

Hata hivyo, katika uamuzi wa mwezi uliopita, Mahakama ya Juu ilisitisha kesi ya raia katika mahakama za kijeshi.

Lakini Rais Yoweri Museveni katika taarifa yake, aliitetea serikali kwa kusema kuwa uendeshaji wa kesi hiyo umechelewa baada ya Mahakama ya juu kuamua kuhamisha kesi hiyo kutoka Mahakama ya Kijeshi na kuipeleka Mahakama ya Kiraia, mchakato unaochukua muda mrefu.

Mahakama Kuu inatarajiwa kutoa uamuzi wa ombi la wawili hao kuhusu kuachiwa kwa dhamana katika siku zijazo.

Wakati huo huo, mashirika ya kutetea haki za binadamu, wanasiasa wa upinzani na viongozi wa kidini wanataka Besigye aachiliwe mara moja.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti