| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Tanzania kujenga Uwanja wa Ndege wa Kimataifa mkoani Mwanza
Akizungumza Bungeni jijini Dodoma Mei 13, 2026, Waziri Mkuu huyo amesema kuwa serikali ya nchi hiyo inatambua umuhimu wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza na imeendelea kufanya jitihada mbalimbali kuhakikisha unakuwa na uwezo wa kuhudumia ndege kubwa pamoja.
Tanzania kujenga Uwanja wa Ndege wa Kimataifa mkoani Mwanza
Waziri Mkuu wa Tanzania, Mwigulu Nchemba./Picha:Wengine / Others

Waziri Mkuu wa Tanzania Mwigulu Nchemba, amesema serikali ya nchi hiyo inaendelea kuchukua hatua kuhakikisha Uwanja wa Ndege wa Mwanza unaboreshwa na kujengwa katika hadhi ya kimataifa ili kuendana na hadhi ya jiji hilo akama kitovu muhimu cha shughuli za kiuchumi Kanda ya Ziwa.

Akizungumza Bungeni jijini Dodoma Mei 13, 2026, Waziri Mkuu huyo amesema kuwa serikali ya nchi hiyo inatambua umuhimu wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza na imeendelea kufanya jitihada mbalimbali kuhakikisha unakuwa na uwezo wa kuhudumia ndege kubwa pamoja na kukidhi viwango vya kimataifa.

“Zipo jitihada ambazo zimekuwa zikifanyika kuhakikisha kwamba uwanja wa ndege wa Mwanza unaendana na hadhi ya Mwanza kama kitovu cha shughuli za kiuchumi Kanda ya Ziwa,” alisema Nchemba.

Aidha, kiongozi huyo ameongeza kuwa nchi hiyo inaendelea na mazungumzo ya kuongeza eneo la uwanja huo ili kuwezesha upanuzi wa njia ya kurukia ndege (runway) pamoja na maboresho mengine muhimu ya miundombinu.

Katika hatua nyingine, Nchemba amesema kuwa serikali ya nchi hiyo imekubaliana kujenga jengo jipya la abiria litakalokuwa na hadhi ya kimataifa na kuendana na mahitaji ya muda mrefu ya uwanja huo.

“Imekuja kukubalika kwamba tujenge jengo ambalo halitahitaji kubomolewa tena baada ya muda mfupi, bali jengo lenye hadhi na viwango vya viwanja vya ndege vya kimataifa,” aliongeza.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Wananchi waelimishwe kuhusu umuhimu wa kuandikishana mikataba ya ardhi-Wazri Mkuu wa Tanzania
Misri, Qatar wasisitiza utekelezaji wa makubaliano ya awamu ya kwanza ya kusitisha mapigano Gaza
DRC kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Chile nchini Ufaransa baada ya marufuku ya Hispania
Afrika Kusini yaishutumu Ghana kufanya 'mbwembwe za umma' wakati wa kurudisha raia wake
Utafiti wa miaka mingi wa kutafuta mnyama anayeeneza virusi vya Ebola
Boko Haram yawaachilia mamia ya watu waliotekwa nyara nchini Nigeria
Askofu wa Msumbiji afariki baada ya kupigwa risasi nyumbani kwake
Mauritius inazuia kuingia kwa wasafiri kutoka nchi zilizokumbwa na Ebola
Utamaduni uliokosea? Jinsi usimamizi wa AI unatishia Usanii wa kimila wa Kiafrika
Janga la Ebola: Wafanyabiashara wapata hasara kubwa katika mpaka wa Uganda-DRC
Mchekeshaji wa Kenya Eric Omondi akamatwa kwa maandamano kupinga kupanda bei ya mafuta
Ebola inaenea 'kwa kasi' huku maambukizi 71 mapya yakithibitishwa katika siku moja
Chama tawala cha Guinea chashinda kwa kishindo bungeni, uchaguzi wa manispaa
Mali yamfunga jela mwanadiplomasia wa Ufaransa kwa madai ya njama ya kuvuruga utulivu
Watu wasiopungua 49 wafariki kwa kiu katika jangwa la Sahara baada ya gari kuharibika Niger
Nigeria kuwasafirisha raia wake zaidi 1,000 kutoka Afrika Kusini
Kiwanda cha mafuta cha Dangote Nigeria chaongeza uwezo, chasafisha mapipa 700,000
Waandamanaji wavamia ofisi ya UN Libya
Mkuu wa Umoja wa Mataifa asikitishwa na ripoti za ghasia katika mji mkuu wa Somalia
Uturuki, Niger watia saini makubaliano ya ushirikiano baada ya mazungumzo ngazi ya urais