| Swahili
ULIMWENGU
1 dk kusoma
Wanafunzi wa Korea Kusini matatani kwa ‘kuvunja’ na kuingia ndani ya kambi ya kijeshi ya Marekani
Wanafunzi hao, wanaume wanne na wanawake wanne, wanadaiwa kuingia ndani ya kambi ya jeshi la anga la Marekani, iliyoko karibu na jiji la Seoul.
Wanafunzi wa Korea Kusini matatani kwa ‘kuvunja’ na kuingia ndani ya kambi ya kijeshi ya Marekani
Kwa upande wake, taarifa ya jeshi la Marekani inadai kuwa wanafunzi hao walijaribu kutumia lango kuu la ngome hiyo yenye ulinzi mkali.

Wanafunzi nane wa Korea Kusini wametiwa nguvuni baada ya kudaiwa kuingia kinguvu ndani ya kambi ya kijeshi ya Marekani.

Wanafunzi hao, wanadaiwa kutoa maneno yenye kuidhihaki Marekani, wakati wa tukio hilo.

Wanafunzi hao, wanaume wanne na wanawake wanne, wanadaiwa kuingia ndani ya kambi ya jeshi la anga la Marekani, iliyoko karibu na jiji la Seoul.

Kulingana na polisi wa nchi hiyo, wanafunzi hao wanadaiwa kupiga kelele za “kuishambulia Marekani”, wakati wakitekeleza tukio hilo.

Kwa upande wake, taarifa ya jeshi la Marekani inadai kuwa wanafunzi hao walijaribu kutumia lango kuu la ngome hiyo yenye ulinzi mkali.

Jeshi la polisi la Korea Kusini, limesisitiza kuwa, suala hilo litashughulikiwa kwa kuzingatia sheria za Marekani na Korea Kusini.

 

CHANZO:AP