| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Jeshi laingia mitaani Johannesburg kukabiliana na magenge ya uhalifu
Hii ni mara ya kwanza kwa idadi kubwa ya wanajeshi kutumwa tangu Rais Cyril Ramaphosa aliposema kuwa magenge ya wahalifu ni tishio kubwa kwa demokrasia Afrika Kusini na maendeleo ya kiuchumi.
Jeshi laingia mitaani Johannesburg kukabiliana na magenge ya uhalifu
Jeshi la Afrika Kusini katika eneo la Riverlea la mji wa Johannesburg, Afrika Kusini. / AP
tokea saa limoja

Wanajeshi wamepelekwa katika mitaa ya mji mkubwa zaidi nchini Afrika Kusini siku ya Jumatani baada ya rais kutangaza mwezi uliopita kuwa ataagiza wanajeshi kusaidiana na polisi katika kukabiliana na vurugu za magenge na uchimbaji haramu wa madini.

Wanajeshi hao wameonekana katika mitaa ya Johannesburg wakianza na Riverlea tangu Rais Cyril Ramaphosa aliposema katika hotuba yake ya kila mwaka kwa taifa kuwa magenge ya wahalifu ni tishio kubwa kwa demokrasia ya Afrika Kusini na maendeleo ya kiuchumi.

Polisi nchini Afrika Kusini na Wizara ya Ulinzi, ambayo inasimamia jeshi, hawakutoa maelezo kuhusu operesheni hiyo.

Nchi hiyo ina kiwango kikubwa cha mauaji karibu watu 60 huuawa kila siku ikiwemo mapigano kati ya magenge ya dawa za kulevya katika maeneo ya mji wa Cape Town na kufyatuliana risasi kunakohusishwa na uchimbaji haramu wa madini katika mji wa mkoa wa Gauteng, Johannesburg.

CHANZO:TRT Afrika Swahili