| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Kiongozi wa upinzani Uganda Bobi Wine atoroka nchini baada ya uchaguzi uliokuwa na mvutano
Kiongozi wa upinzani Bobi Wine anathibitisha kuwa ametoroka nchini Uganda, lakini hakufichua alipokwenda, baada ya kujificha kwa muda kwa kuhofia maisha yake.
Kiongozi wa upinzani Uganda Bobi Wine atoroka nchini baada ya uchaguzi uliokuwa na mvutano
Rais Yoweri Museveni wa Ugandan alishinda kwa asilimia 71.6 ya kura, kwa mujibu wa matokeo ambayo Wine ameyakataa. / AP
15 Machi 2026

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda Bobi Wine amesema Jumamosi kwamba ameikimbia nchi kuepuka msako wa jeshi baada ya Uchaguzi wa urais wa nchi hiyo.

Wine, ambae jina lake halisi ni Kyagulanyi Ssentamu, alikuwa mafichoni muda mfupi tu baada ya Uchaguzi wa Januari 15.

Rais Yoweri Museveni wa Ugandan alishinda kwa asilimia 71.6 ya kura, kwa mujibu wa matokeo ambayo Wine ameyakataa.

Kwa wiki kadhaa, sehemu aliyokuwa amejificha Bobi Wine haijulikana, huku kukiwa na wasiwasi kuhusu usalama wake baada ya Mkuu wa Majeshi, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, mara kadhaa kutoa vitisho dhidi yake kupitia mtandao wa X.

Kainerugaba, mtoto wa Rais, alisema Wine anatafutwa kwa makosa ambayo hayakutajwa. Polisi nchini Uganda inasema haimtafuti.

Katika ujumbe wa video iliyowekwa katika mtandao wa X Jumamosi, Wine alisema kuwa amefanikiwa kuondoka Uganda lakini hakutaja sehemu alipo.

“Waganda wenzangu na marafiki zangu wa Uganda duniani kote, mpaka muda huu mnapoona video hii, itakuwa nimeondoka Uganda kwa majukumu muhimu nje ya Uganda,” amesema.

‘Nitarudi’

“Na kwa muda sahihi nitarudi na kuendelea na mapambano. Nawashukuru nyote Waganda wenzangu walionificha na kunilinda muda wote huo wakati utawala ulipokuwa unanitafuta."

Amesema isingewezekana kwa vikosi vya Uganda kumpata "kwa sababu watu walinilinda."

Wanajeshi wa Uganda walivamia nyumba ya Wine siku moja baada ya Uchaguzi wa Januari 15, lakini kiongozi huyo wa upinzani alikuwa tayari ameshaondoka, akihofia maisha yake baada ya wiki kadhaa za kampeni akiwa amevaa 'helmet' katika mikutano ambayo mara nyingi ilihudhuriwa na vikosi vya ulinzi.

Wine, mgombea maarufu katika wagombea saba waliosimama dhidi ya Museveni, alivutia zaidi vijana maeneo ya mijini.

Mwezi Mei, Museveni mwenye umri wa miaka 81 ataapishwa kwa muhula wa saba ambao utamfanya aendelee kuwa madarakani kwa karibu miongo mitano.

Wafuasi wake wanamsifu kwa kuleta amani na utulivu ambapo Uganda imekuwa makazi ya maelfu ya wakimbizi kutoka nyengine za Afrika. Lakini viongozi wa upinzani, wakiwemo baadhi waliokuwa washirika wake wa karibu, wanamlaumu kwa kile wanachokiona kama ukandamizaji wa demokrasia.

Soma zaidi
Watu kumi na nne waliotekwa Nigeria waokolewa: Gavana wa Jimbo
Ziara ya Afrika: Papa Leo afanya Misa nchini Angola
Wamefukuzwa Sahel: Ufaransa inatafuta nini nchini Kenya?
Pande zinazopigana DR Congo zimekubaliana kubadilishana wafungwa na kuruhusu ufikiaji wa msaada
Nigeria yavamia ‘kiwanda cha watoto’ huko Lagos, na kuwaokoa wanawake wajawazito
Marekani yawawekea vikwazo wapiganaji wa Colombia nchini Sudan
Kundi la kwanza la waliofukuzwa kutoka Marekani lawasili Kinshasa nchini DRC
Mtoto wa Mugabe akiri kumtishia mtu kwa bunduki nchini Afrika Kusini
Nigeria yapiga marufuku kusimikwa kwa ‘Wafalme wa Igbo’ nje ya nchi
Mawaziri wa mambo ya nje wa Uturuki, Misri, Pakistan, Saudia kukutana Jukwaa la Diplomasia Antalya
Somalia inasema hatua ya Israel kuunga mkono Somaliland inakiuka Uhuru wa Somalia
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Somalia yashtumu uteuzi wa balozi wa Israel katika eneo lililojitenga la Somaliland
Uganda inasema inahitaji zaidi ya Dola bilioni moja kusambaza umeme nchini kote
Afrika Kusini yampa kifungo cha miaka mitano jela Julius Malema kwa kufyatua risasi