| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Mkuu wa ujasusi wa Uturuki, Ibrahim Kalin akutana na mwenzake wa Ugiriki mjini Athens
Mkuu wa Ujasusi wa Uturuki (MIT), Ibrahim Kalin, na Mkuu wa Ujasusi wa Ugiriki (EYP), Themistoklis Demiris, wamejadili masuala ya mataifa mawili na ya kikanda, na kukubaliana kuimarisha zaidi ushirikiano katika nyanja ya ujasusi.
Mkuu wa ujasusi wa Uturuki, Ibrahim Kalin akutana na mwenzake wa Ugiriki mjini Athens
Mkuu wa Ujasusi wa Uturuki, Ibrahim Kalin. / AA / AA

Mkuu wa Ujasusi wa Uturuki (MIT), Ibrahim Kalin, amekutana na Mkuu wa Ujasusi wa Ugiriki (EYP), Themistoklis Demiris, mjini Athens wiki iliyopita, kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vya usalama.

Katika mkutano huo, Kalin na Demiris walijadili uhusiano wa mataifa hayo mawili pamoja na yanayojiri katika kanda, huku pande hizo mbili zikitathmini hatua zinazoweza kuchukuliwa ili kushughulikia masuala yaliyopo, iliripoti TRT Haber.

Mazungumzo hayo yalisisitiza umuhimu mkubwa wa uhusiano kati ya Uturuki na Ugiriki katika maeneo mbalimbali, yakiwemo Bahari ya Aegean na Mediterania ya Magharibi, usalama wa NATO, ushirikiano wa kijasusi, pamoja na juhudi za kukabiliana na ugaidi, uhalifu uliopangwa, uhamiaji harari na biashara haramu ya kusafirisha watu.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mazungumzo hayo pia yaliangazia vita vya Marekani dhidi ya Iran, enzi mpya nchini Syria, umoja wa kisiasa wa Libya, vita vya Israel dhidi ya Gaza pamoja na ukiukaji unaoendelea na sera za Israel za kukalia maeneo katika Ukingo wa Magharibi . Aidha, pande hizo zilijadili mashambulizi ya Israel dhidi ya Syria na Lebanon.

Pande zote mbili zilikubaliana kuhusu umuhimu wa kudumisha na kuendeleza kasi iliyopatikana hivi karibuni katika mapambano dhidi ya ugaidi na makundi ya uhalifu uliopangwa, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano huo kufikia kiwango cha kimkakati.

Kalin wa MIT na Demiris wa EYP pia walikubaliana kuimarisha zaidi ushirikiano wa karibu kati ya mashirika hayo mawili ya kijasusi katika masuala ya nchi mbili na masuala ya kikanda.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Uturuki kuongeza ushirikiano na Muungano wa Ushirikiano wa Shanghai: Rais Erdogan
Mkataba wa Ulinzi wa Makkah waweka msingi wa kujenga mfumo mpya wa usalama wa kikanda: Fidan
Uturuki, Pakistan na Saudi Arabia kufanya mkutano wa kwanza wa makubaliano ya ulinzi ya Makka
Operesheni ya uokoaji inaendelea baada ya kivuko kupinduka karibu na TRNC
Agosti 30: Ushindi uliofungua njia ya kuinuka kwa Uturuki ya kisasa
Erdogan ameisifu Uturuki katika maadhimisho ya miaka 104 ya 'Siku ya Ushindi'
Jeshi la Wanamaji la Uturuki na vikosi vya Somalia vyaokoa meli ya mizigo iliyotekwa na maharamia
Uturuki yataka kupunguza mizozo katika Ulimwengu wa Kiislamu: Erdogan
Rais Erdogan ajadili amani ya kikanda na viongozi wa Rwanda na DRC
Erdogan: Uturuki itaendelea kufanya maendeleo licha ya migogoro ya kikanda
Erdogan na Lula wajadili kuimarisha zaidi uhusiano wa kiuchumi
Katika picha: Waogeleaji 2,500 wavuka Mlango-bahari wa Istanbul katika mbio za kila mwaka za mabara
Uturuki yataka ilani nyekundu ya Interpol dhidi ya Netanyahu kufuatia shambulio dhidi ya fotilla
Uturuki kuimarisha uwezo wa jeshi lake la wanamaji: Waziri wa Ulinzi
Waziri wa zamani wa ulinzi wa Israel Yaalon amshtumu Netanyahu kwa uchokozi dhidi ya Uturuki
Uturuki itaendelea kuwa chanzo cha matumaini kwa Gaza na dunia: Erdogan
Kenya, Uturuki kushirikiana zaidi katika biashara, uwekezaji na ulinzi
Uturuki yachapisha rasmi sheria ya mchakato wa 'Uturuki Isiyo na Ugaidi'
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki afanya mazungumzo na mawaziri wenzake wa Qatar na Syria
Chombo cha Uturuki cha Marlin chaimarisha uwezo wa kutegesha mabomu baharini