| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Wasira wa CCM awataka vijana kutotumika kuiharibu Tanzania
Tanzania inatarajia kufanya Uchaguzi wake Mkuu Oktoba 29, 2025 ambapo wananchi wa taifa hilo wanatumia haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi mbalimbali, kuanzia rais, wabunge na madiwani.
Wasira wa CCM awataka vijana kutotumika kuiharibu Tanzania
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Stephen Wasira./Picha:@ccm_tanzania
17 Oktoba 2025

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amewataka vijana kukataa kutumika kwa maslahi ya wengine wenye nia ovu, huku akiwahakikishia wananchi kuwa uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025 unafanyika kwa amani na salama.

Kulingana na Wasira, yapo baadhi ya mashirika ya kimataifa yanatamani kuona amani iliyopo nchini humo inavurugika, akiwahahakishia kuwa chama hicho kimesimama imara kulinda amani, umoja na mshikamano wa Watanzania.

"Nataka niwaambie Watanzania uchaguzi utafanyika tarehe 29 tena kwa amani, na yule ambaye anaota amani itapotea anapoteza wakati wake, kwa sababu CCM bado tunashikilia dola, amani itakuwa tele, waambieni wapigakura hakuna mtu atakayefanya chochote,” alisema Wasira.

Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, alibainisha kuwa yapo baadhi ya mashirika ya kimataifa yasiyotaka kuona amani inaendelea kuwepo nchini humo na kuwa yapo tayari kutoa fedha kuvuruga utulivu wa Watanzania.

"Yapo baadhi ya mashirika ya kimataifa yana matatizo na mengine hayataki kuona amani ya nchi yetu, yapo tayari kutoa fedha ili amani itoweke," ameeleza.

Aidha, Wasira amewataka vijana wakatae kutumika kuleta vurugu kwa kuwa ustawi wa maendeleo yao na nchi kwa ujumla unategemea amani na utulivu.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti
Nigeria yaanzisha uchunguzi baada ya kukamata kilo 1,000 za kokeini yenye thamani ya $235M
Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam
Mtoto wa Gaddafi aachiliwa huru baada ya miaka kumi gerezani
Kuanzia vifo vya taratibu hadi mauaji ya ukatili: Kutoweka kwa utu Al Fasher
Zaidi ya mataifa 20 yanalaani ukatili wa RSF nchini Sudan, na kutaka kukomeshwa kwa ghasia
Rais wa Misri, afisa mkuu wa usalama wa Urusi kujadili ushirikiano wa kijeshi
Maelfu ya wananchi wanashikiliwa katika hali mbaya sana katika Al Fasher, Sudan: madaktari
Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aghairi ziara iliyopangwa nchini Kenya
‘Mauaji ya waandamanaji ni chukizo mbele za Mungu’
Jeshi la Sudan lazima shambulio la RSF katika mji wa Babnousa huko Kordofan Magharibi
Majeshi ya Somalia yawaua viongozi watatu wakuu wa Al Shabaab
Rwanda, DRC zaanzisha mfumo wa ushirikiano wa kiuchumi huku kukiwa na mazungumzo ya amani
RSF yazika miili katika makaburi ya halaiki, inachoma wengine ili 'kuficha ushahidi wa mauaji
Wananchi katika Al Fasher, Sudan, wanakabiliwa na ukatili 'wa kiwango kisichoweza kuaminika' — UN
Chama tawala nchini Djibouti kimemteua Rais Guelleh kwa muhula wa sita
Amaan Golugwa akamatwa huku polisi Tanzania ikiwasaka viongozi wa upinzani kufuatia maandamano
Wafanyakazi waokolewa baada ya maharamia kushambulia meli ya mafuta kutoka Somalia