| swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Wasira wa CCM awataka vijana kutotumika kuiharibu Tanzania
Tanzania inatarajia kufanya Uchaguzi wake Mkuu Oktoba 29, 2025 ambapo wananchi wa taifa hilo wanatumia haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi mbalimbali, kuanzia rais, wabunge na madiwani.
Wasira wa CCM awataka vijana kutotumika kuiharibu Tanzania
Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Stephen Wasira./Picha:@ccm_tanzania
17 Oktoba 2025

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amewataka vijana kukataa kutumika kwa maslahi ya wengine wenye nia ovu, huku akiwahakikishia wananchi kuwa uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025 unafanyika kwa amani na salama.

Kulingana na Wasira, yapo baadhi ya mashirika ya kimataifa yanatamani kuona amani iliyopo nchini humo inavurugika, akiwahahakishia kuwa chama hicho kimesimama imara kulinda amani, umoja na mshikamano wa Watanzania.

"Nataka niwaambie Watanzania uchaguzi utafanyika tarehe 29 tena kwa amani, na yule ambaye anaota amani itapotea anapoteza wakati wake, kwa sababu CCM bado tunashikilia dola, amani itakuwa tele, waambieni wapigakura hakuna mtu atakayefanya chochote,” alisema Wasira.

Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, alibainisha kuwa yapo baadhi ya mashirika ya kimataifa yasiyotaka kuona amani inaendelea kuwepo nchini humo na kuwa yapo tayari kutoa fedha kuvuruga utulivu wa Watanzania.

"Yapo baadhi ya mashirika ya kimataifa yana matatizo na mengine hayataki kuona amani ya nchi yetu, yapo tayari kutoa fedha ili amani itoweke," ameeleza.

Aidha, Wasira amewataka vijana wakatae kutumika kuleta vurugu kwa kuwa ustawi wa maendeleo yao na nchi kwa ujumla unategemea amani na utulivu.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
UN yaagiza uchunguzi wa dharura ufanyike kuhusu ukiukaji wa sheria katika Al Fasher ya Sudan
Rais wa Tanzania atangaza uchunguzi kuhusu mauaji ya waandamanaji katika uchaguzi
Wakimbizi 57,000 wamewasili kaskazini mwa Sudan baada ya mashambulizi ya RSF huko Darfur, Kordofan
Afrika Kusini yaruhusu kuingia kwa wakimbizi zaidi ya 150 kutoka Gaza, Palestina
Afrika yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu mbaya zaidi katika miaka 25
Mataifa ya G7 walaani mashambulizi ya RSF dhidi ya raia Sudan, watoa wito wa kusitishwa mapigano
Wakenya zaidi ya 200 wajiunga na jeshi la Urusi
AU yakanusha tuhuma za Trump kuhusu mauaji ya halaiki Nigeria
Mwigulu Nchemba ateuliwa Waziri Mkuu Tanzania
Jaji Mkenya achaguliwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amfuta kazi makamu wake
Duma wa Botswana aipa India zawadi ya duma 8
Kesi ya Roger Lumbala wa DRC yaanza kusikilizwa
Kesi za ubakaji, watoto kupotea zaripotiwa Darfur, Sudan – Umoja wa Mataifa
Ugonjwa wa Kichaa cha mbwa barani Afrika: Janga linaloendelea kuathiri maisha japo linaepukika
Libya yatakiwa kufunga vituo vya kuwazuilia wahamiaji katika mkutano wa Umoja wa Mataifa
Rais Museveni aonya kuzuka kwa vita endapo nchi za Afrika zitashindwa kufikia Bahari ya Hindi
UN: Milioni 11 wanawake na wasichana wanabeba uzito mkubwa wakati njaa ya Sudan inaendelea kupamba moto
Ethiopia yachagguliwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya hewa, COP32
Ghana yafichua sababu ya ajali ya helikopta iliyoua watu wanane, wakiwemo mawaziri, mwezi Agosti