| Swahili
ULIMWENGU
2 dk kusoma
Rais Trump awafukuza raia wa Zimbabwe na Ghana kutoka Marekani hadi Cameroon
Inaripotiwa kuwa wahamiaji hao waliwasili katika mji mkuu wa Cameroon, Yaoundé, siku ya Jumatatu, wiki chache tu baada ya wahamiaji wengine tisa kupelekwa huko kimyakimya kufuatia sera ya Trump dhidi ya wahamiaji.
Rais Trump awafukuza raia wa Zimbabwe na Ghana kutoka Marekani hadi Cameroon
Rais Donald Trump akizungumza na waandishi wa habari ndani ya ndgege ya Air Force One. / / AP
18 Februari 2026

Ndege nyingine ya kuwafukuza wahamiaji kutoka Marekani imetua nchini Cameroon. Hata hivyo, waliorejeshwa si raia wa Cameroon na, kulingana na mawakili wao, hawana uhusiano wowote na nchi hiyo.

Kundi la hivi karibuni la wahamiaji linaripotiwa kuwasili Yaoundé siku ya Jumatatu, tarehe 16 Februari, wiki chache baada ya wahamiaji wengine tisa kupelekwa huko kimyakimya kufuatia sera yenye utata ya Trump ya kuwafukuza wahamiaji.

Ingawa utaifa wa wahamiaji wa hivi karibuni haukufahamika papo hapo, kundi la kwanza lilijumuisha wanawake watano na wanaume wanne kutoka nchi kama Zimbabwe, Morocco na Ghana, kulingana na ripoti za vyombo vya habari.

Mawakili wao, Alma David nchini Marekani na Joseph Awah Fru nchini Cameroon, waliiambia shirika la habari la The Associated Press kuwa kuwafukuza wahamiaji hao kwenda Cameroon kulikiuka maagizo ya mahakama za Marekani yaliyowapa ulinzi dhidi ya kufukuzwa.

Ikulu ya Marekani imethibitisha safari hiyo ya hivi karibuni ya ndege lakini haijatoa maelezo zaidi.

Mikataba ya siri

Cameroon si nchi pekee ya Afrika ambayo serikali ya Trump imepeleka wahamiaji kutoka nchi za dunia ya tatu. Katika miezi iliyopita, Marekani imewapeleka katika nchi za Sudan Kusini, Rwanda, Ghana, Uganda, Eswatini na Guinea ya Ikweta, kati ya waliorejeshwa wengine siyo wa kutoka nchi za Afrika.

Uhamisho huo, ambao ni sehemu ya msako mkali wa Trump dhidi ya wahamiaji, hufanywa chini ya mikataba yenye utata na mara nyingi ya siri, ambapo Marekani hulipa nchi zinazowapokea ili kuwahudumia wahamiaji ambao si raia wao.

Ripoti ya Kamati ya Mahusiano ya Kigeni ya Seneti ya Marekani inakadiria kuwa utawala wa Trump umetumia angalau dola milioni 40 kuwahamisha takriban wahamiaji 300 kwenda nchi zisizo zao.

Idara ya Mambo ya Nje ya Marekani pia ilisema kuwa Eswatini itapokea dola milioni 5.1 ili kupokea hadi wahamiaji 160 kutoka nchi za tatu.

Wahalifu waliotiwa hatiani Marekani

Mwaka jana, wanaume watano kutoka Vietnam, Jamaica, Cuba, Yemen na Laos, waliopatikana na hatia ya makosa makubwa nchini Marekani, walifukuzwa na kupelekwa Eswatini.

Ingawa nchi nyingi zinazowapokea wahamiaji hazijatoa maelezo ya kina, Ghana ilikanusha kupokea malipo kwa kuwahifadhi wahamiaji mwaka jana, ikisema hatua yake ilitokana na “roho ya Uanamajumui” (Pan-African spirit).

Marekani inadai kuwa inatekeleza sheria za uhamiaji, lakini wahamiaji waliorejeshwa na wanaharakati wanasema kuwa hatua hiyo ni ukiukaji wa haki za binadamu, kwa kuwa baadhi yao walikimbia nchi zao kutokana na hofu za usalama, na kufukuzwa kwao hakukufuata utaratibu unaostahili wa kisheria.

Raia wa nchi zinazowapokea pia wana hofu kuwa mara nyingi wahalifu sugu hujumuishwa miongoni mwa waliorejeshwa.

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Takriban watu 30 wamefariki katika mkanyagano kwenye ngome ya kihistoria ya Laferriere nchini Haiti
Hakuna makubaliano ya Marekani-Iran baada ya mazungumzo ya saa 21 nchini Pakistan, asema Vance
Marekani yakubali kuachilia mali ya Iran iliyozuiliwa ili kuendeleza mazungumzo ya Islamabad
Makamu wa Rais Vance awasili Pakistan kuanza mazungumzo muhimu ya Marekani na Iran
Korea Kaskazini, China zakutana, kukuza ushirikiano wa kimkakati
Rais Macron, Papa Leo wa 14 wajadili hali ya Mashariki ya Kati
Netanyahu asema Israel itaishambulia Hezbollah pale inapobidi
Kocha wa zamani wa Romania Mircea Lucescu afariki dunia
Bilionea Bill Gates kutoa ushahidi wake kuhusu faili za Jeffrey Epstein
Netanyahu: Tumeshambulia reli na madaraja ya Iran
Mbunge wa Marekani aanza mchakato wa kura ya kutokuwa na imani dhidi ya Waziri wa Ulinzi
Misri, Uturuki na Pakistan katika jitihada za upatanishi: Vyombo vya habari Marekani
Trump aongeza shinikizo kwa Iran, atishia hatua kali iwapo hakutakuwa na makubaliano
Trump: Mitambo ya umeme ya Iran, madaraja yatapigwa iwapo Bahari ya Hormuz haikufunguliwa
Wataalam 100 wanaonya kuwa mashambulizi ya Marekani dhidi ya Iran yanaweza kuwa uhalifu wa kivita
Afisa wa Marekani athibitisha kudunguliwa kwa ndege ya Marekani nchini Iran
Kiongozi wa mapinduzi ya Myanmar ashinda kiti cha Urais
Tetemeko la ardhi la kiwango cha 7.4 laua mtu mmoja Indonesia na kusababisha tahadhari za tsunami
Trump afikiria kuiondoa Marekani kutoka NATO
UAE inaunga mkono hatua ya kijeshi ya kufungua tena Mlango-Bahari wa Hormuz