| Swahili
ULIMWENGU
1 dk kusoma
Wanajeshi wanne wa Israel wameuawa Lebanon
Vifo hivi vinatokea wakati Israel ikifanya mashambulizi ya anga na ardhini kusini mwa Lebanon, baada ya shambulizi la Hezbollah dhidi ya Israel la Machi 2.
Wanajeshi wanne wa Israel wameuawa Lebanon
Wanajeshi wa Israel wakusanyika karibu na mpaka wa Israel-Lebanon kaskazini mwa Israel, Machi 30 2026. / / Reuters
tokea masaa 12

Wanajeshi wanne wa Israel wameuawa na wengine wawili kujeruhiwa katika mapigano kusini mwa Lebanon, Jeshi la Israel limesema siku ya Jumanne.

Vifo hivi vinatokea wakati Israel ikifanya mashambulizi ya anga na ardhini kusini mwa Lebanon, baada ya shambulizi la Hezbollah dhidi ya Israel la Machi 2.

Kilichoanza kama mzozo wa kieneo, sasa limegeuka kuwa operesheni ya kuendelea, huku makabiliano ya mabomu na risasi yakiendelea karibu kila siku.

Idadi ya raia waliouawa yaongezeka Lebanon

Nchini Lebanon, angalau watu 1,247 wameuawa na 3,690 kujeruhiwa, kwa mujibu wa maafisa, tangu mashambulizi ya Israel yaanze, huku mashambulizi yakiathiri miji na miundombinu kusini mwa nchi hiyo.

Kuongezeka kwa mapigano kunahusiana na operesheni pana zaidi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, ambayo imeua zaidi ya watu 1,340 tangu mwishoni mwa Februari, kwa mujibu wa maafisa wa Iran.

Kwa kijibu mashambulizi hayo, Iran imezindua wimbi la mashambulizi ya ndege zisizo na rubani na makombora dhidi ya Israel na kambi za kijeshi za Marekani katika nchi za Ghuba.

CHANZO:TRT World and Agencies