| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Sudan yashtumu mashambulizi ya RSF yaliyowaua wanafunzi wa kike
Mashambulizi hayo katika shule moja ya sekondari ya kijijini na kituo cha afya yamewaua watu wasiopungua 17.
Sudan yashtumu mashambulizi ya RSF yaliyowaua wanafunzi wa kike
Mtandao wa Madaktari wa Sudan unasema miongoni mwa walioathirika ni wanafunzi wa kike, walimu na wahudumu wa afya. / AP
13 Machi 2026

Serikali ya Sudan imeshtumu mashambulizi ya ndege isiyokuwa na rubani yaliyowaua raia wasiopungua 17 katika kijiji cha Shukeiri Jimbo la White Nile State, ikiilaumu wapiganaji wa RSF kwa shambulio hilo.

Katika taarifa, Waziri Mkuu Kamil Idris na maafisa wa serikali wamelitaja shambulio hilo kuwa la kikatili.

“Waziri Mkuu, Profesa Kamil Idris, na maafisa wa Serikali wanaeleza kusikitishwa kwao na kutuma salamu za rambirambi kwa mauaji ya mashahidi katika kijjiji cha Shukeiri Jimbo la White Nile, ambao roho zao zilichukuliwa kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhan kutokana na mashambulizi yaliyofanywa na waasi na magaidi wa RSF,” kulingana na taarifa iliyotolewa na Shirika la Habari la Sudan.

Serikali inasema mashambulizi hayo yalilenga raia katika kijiji hicho na kutoa wito kwa jamii ya kimataifa kuwawajibisha RSF.

‘Wanashambulia raia kwa makusudi’

Shambulio hilo lililenga shule ya sekondari na kituo cha afya huko Shukeiri siku ya Jumatano,na kuwaua watu wasiopungua 17, wengi wakiwa wanafunzi wa kike, na kuwajeruhi karibu watu 10, kulingana na maafisa wa afya.

Mtandao wa Madaktari wa Sudan unasema miongoni mwa walioathirika ni wanafunzi wa kike, walimu na wahudumu wa afya. Kundi hilo limeshtumu RSF kwa kushambulia kwa makusudi maeneo ya raia.

CHANZO:TRT Afrika Swahili
Soma zaidi
Mwakilishi Maalumu wa Jumuiya ya Madola Lazarus Chakwera ahitimisha ziara yake nchini Tanzania
Kenya yaomba msaada wa haraka kutoka Benki ya Dunia huku ikipunguza VAT
Wadau wajadili fursa za uwekezaji katika Kongamano la Biashara linaloendelea Kigoma, Tanzania
Mbunge Tanzania ataka sekta binafsi iruhusiwe uzalishaji wa nishati ya umeme
Kampuni ya BP yashtakiwa Kenya kufuatia madai ya uchafuzi mazingira kutokana na uchimbaji mafuta
Mashirika ya ndege ya Nigeria yatishia kusitisha huduma kuanzia Aprili 20 kutokana na bei ya mafuta
Somalia yashtumu uteuzi wa balozi wa Israel katika eneo lililojitenga la Somaliland
Uganda inasema inahitaji zaidi ya Dola bilioni moja kusambaza umeme nchini kote
Afrika Kusini yampa kifungo cha miaka mitano jela Julius Malema kwa kufyatua risasi
DRC inaanzisha hifadhi ya kimkakati ya kobalti na madini mengine
Afrika Kusini yamkamata mwanaharakati wa Benin Kemi Seba kwa tuhuma za uchochezi
Burkina Faso yafuta takriban asasi 100 za kiraia
Rais wa Cameroon anasema dunia inahitaji 'ujumbe wa amani' wa Papa
Jeshi la Tanzania latangaza nafasi ajira
Raia wa China ahukumiwa jela kwa kusafrisha mchwa kutoka Kenya kinyume cha sheria
Iran yatishia kuzuia usafiri wa meli katika Bahari ya Shamu ikiwa vikwazo vya Marekani vitaendelea
Marie-Louise Eta: Mwanamama aliyepewa mikoba Bundesliga
Mamia wajitokeza Afrika Kusini kabla ya hukumu ya kifungo cha mwanasiasa Malema
Wasichana ndio waathirika wakubwa zaidi katika vita vilivyosahaulika vya Sudan
Bei ya mafuta yapanda Kenya huku usambazaji ukisuasua