| Swahili
AFRIKA
1 dk kusoma
Mwalimu Mkenya aripotiwa kuuwawa Tanzania
John Okoth Ogutu, Mkenya mwenye umri wa miaka 33 aliyeishi Tanzania kwa zaidi ya miaka kumi, ameripotiwa kuuawa kwa risasi wakati wa machafuko yaliyotokea Dar es Salaam baada ya uchaguzi.
Mwalimu Mkenya aripotiwa kuuwawa Tanzania
Familia ya Ogutu iko mbioni kupata taarifa zaidi kuhusu sehemu mwili ulipo. / / Wengine
5 Novemba 2025

Kwa mujibu wa familia yake, waliarifiwa kuwa Ogutu, aliyekuwa akifundisha katika Shule ya Msingi ya Sky School, alipigwa risasi jijini Dar es Salaam wakati polisi walipowafyatulia risasi waandamanaji waliokuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi wa Oktoba 29.

Aidha mwili wake unaripotiwa kuhifadhiwa katika hospitali moja jijini humo na familia yake iko mbioni kupata taarifa zaidi kuhusu sehemu mwili ulipo.

“Vita vimenza tukapata habari kwamba amepigwa risasi," Jennifer Otieno, dada yake John Okoth Ogutu amesema.

Naye kaka yake Benard Brian ameongeza ya kuwa: “Tumepatwa na huzuni sana. Kwa wale Wakenya walienda kibiashara, hivi sasa taarifa ambazo tunapata ni kwamba Wakenya wanadhulumiwa. Wakenya wamewekwa kama wahalifu. Ndugu yetu hakuwa mhalifu.”

Licha ya juhudi za kutafuta taarifa, ikiwemo kuwasiliana na Wizara ya Mambo ya Nje ya Kenya na kufika Ubalozi wa Tanzania, familia imesema haijapokea maelezo yoyote kuhusu mipango ya kurejesha mwili au hali ya Wakenya wengine waliokumbwa na vurugu hizo.

InayohusianaTRT Afrika - SADC yakosoa mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa Tanzania

CHANZO:TRT Afrika
Soma zaidi
Afrika Kusini yaomba utulivu kufuatia maandamano dhidi ya kusimikwa kwa 'Igwe' wa Nigeria
Rwanda ‘yahofia’ operesheni za DRC dhidi ya kikundi cha FDLR
Kenya yalipa ada ya Dola milioni 30 ya uenyeji wa AFCON 2027
Hasara ya mamilioni kufuatia ubomoaji katika soko kubwa zaidi la wazi la Gikomba Nairobi
Shabiki maarufu ‘Lumumba Vea’ akosa viza ya  kwenda kuishangilia DRC dhidi ya Jamaica
Mamlaka ya uchukuzi Kenya yazindua ukaguzi wa lazima wa afya kwa madereva ili kupunguza ajali
Tanzania yahimiza matumizi ya AI kuimarisha mtangamano na maendeleo EAC
Kundi lenye silaha limewaua watu wasiopungua 20 Jimbo la Plateau nchini Nigeria
Wafungwa wasiopungua 11 wafariki kutokana na mlipuko wa kipindupindu katika jela DRC
Kagame awaamuru maafisa waandamizi wa serikali 'kusimama' wakati wa hotuba yake
Wadukuzi wadukua maombi ya kazi 450,000 nchini Afrika Kusini
Rais wa Misri asema ni Trump pekee anaweza kusimamisha vita, aonya kupanda zaidi kwa bei ya mafuta
Togo yatoa uzoefu wa kupambana na magonjwa yasiyopewa kipaumbele
Watu 15 wamefariki katika ajali ya barabarani mkoa wa kati Kenya
Mahakama kuu ya Jamhuri ya Congo imethibitisha ushindi wa Sassou Nguesso kwa awamu ya tano
Rwanda, Burundi wanagombana juu ya juhudi za rais wa zamani wa Senegal Sall kuongoza UN
Vifo kutokana na mafuriko nchini Kenya vyaongezeka hadi 108, polisi wasema
Majenerali wakuu wa Uganda wazuiliwa kwa madai ya ufisadi: ripoti
Eswatini yamrudisha nyumbani mwananchi wa Cambodia aliyefukuzwa kutoka Marekani
Waasi waanza kuondoka katika vijiji vya DRC ili kuhimiza amani