| Swahili
AFRIKA
2 dk kusoma
Mwendesha Mashtala wa ICC asimamishwa kazi kwa madai ya dhulma za ngono
Karim Khan atafikishwa kwa kamati ya nidhamu ambayo inawakilishwa na mataifa wanachama 125, kulingana na ICC.
Mwendesha Mashtala wa ICC asimamishwa kazi kwa madai ya dhulma za ngono
Picha: Mahmoud Hjaj / AA

Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya ICC Karim Khan amesimamishwa kazi kuanzia Jumatatu kufuatia uchunguzi wa madai ya dhulma za ngono.

ICC ilitangaza uamuzi huo, ikisema Khan atafikishwa kwa kamati ya nidhamu ambayo inawakilishwa na mataifa wanachama 125 kufuatia matokeo ya uchunguzi wa Umoja wa Mataifa, ambao haujawekwa wazi kwa umma.

"Tathmini ya ICC ni kulingana na ripoti ya uchunguzi uliofanywa na Ofisi ya Umoja wa Mataifa (OIOS), ushahidi uliopo, ushauri wa kamati ya wataalamu wa sheria, na ushahidi wa maandishi," ICC ilisema katika taarifa.

"Uamuzi wa ICC na nyaraka zingine utabaki kuwa siri. Mahakama imetoa wito wa kuheshimiwa kwa faragha na haki za pande zote zinazohusika, pamoja na kuzingatia mchakato unaoendelea," iliongeza.

Mkutano mkuu utalishughulikia suala hilo "mara moja."

Khan, ambaye alienda likizo Mei 2025 wakati uchunguzi wa Umoja wa Mataifa ukiendelea , alisema mwezi Aprili kuwa “ameondolewa lawama.”

Khan aliliambia shirika la habari la Zeteo katika mahojiano kuwa uchunguzi huo hawakumpata “na makosa ya dhulma za ngono au matumizi mabaya ya mamlaka” na kwamba anatakiwa kuruhusiwa kurudi kazini.

“Nimeisoma ripoti ya Umoja wa Mataifa. Nimesoma matokeo ya uchunguzi wa majaji. Na katika ripoti ya Umoja wa Mataifa, kuna ripoti za uchunguzi 137. Hakuna hata moja ambayo inaonesha makosa kwa njia yoyote ile ,” alisema.

Mwezi Machi, jopo la majaji watatu lilikubaliana kwa pamoja kuwa matokeo ya uchunguzi wa Umoja wa Mataifa “hayana msingi wa makosa au ukiukwaji wa majukumu kwa mujibu wa sheria zilizopo,” kulingana na shirika la Middle East Eye.

Uchunguzi huo ulianzishwa na Mkuu wa Baraza la ICC, mwezi Novemba 2024 baada ya mfanyakazi katika ofisi ya Khan kumshtumu kwa madai ya dhulma za ngono.

Mwezi Agosti, mwaka uliopita mwanamke wa pili alijitokeza, akidai mwendesha mashtaka alitumia vibaya mamlaka yake wakati akifanya kazi katika ofisi yake.

Madai hayo yanakuja huku ofisi ya Khan ikifuatilia madai ya uhalifu wa kivita na mauaji ya halaiki ya maafisa wa Israel na wanajeshi huko Gaza na maeneo ya Palestina yanayokaliwa.

Mwezi Mei 2024, Khan alitangaza kuwa atatoa hati za kukamatwa kwa Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na waziri wake wa ulinzi wakati huo, Yoav Gallant, kuhusiana na "uhalifu" kwa madai ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu Gaza.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Waandamanaji nchini Afrika Kusini wanavamia nyumba hadi nyumba kuwasaka wahamiaji
Morocco yaahidi kujiimarisha zaidi baada ya kutolewa Kombe la Dunia
Benki ya Dunia: Wakenya milioni 2.4 wako hatarini kutumbukia kwenye umaskini
Aliyekuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ali Khamenei azikwa, huku waombolezaji waapa kulipiza kisasi
Urusi kuisaidia Msumbiji kupambana na ugaidi
Tanzania: Watu 130 wakamatwa kwa kuhamasisha vitendo vya kihalifu
Marekani yashambulia daraja muhimu la reli linalounganisha Iran, China na Urusi
Morocco iko imara kuliko Paraguay: Kocha wa Ufaransa Deschamps
Vifo vya Ebola vyafikia 600 nchini DRC huku maambukizi yakiripotiwa katika jimbo jipya
CCM na ACT-Wazalendo wamaliza mgogoro wa kisiasa Zanzibar
Somalia yapongeza upatanishi wa Uturuki baada ya upinzani kukubali mazungumzo ya katiba
Iran yaionya Marekani baada ya mashambulizi mapya, yasema ni Iran pekee itakayoamua hatima ya Hormuz
Tanzania yanunua zaidi ya tani 28 za dhahabu ili kuongeza akiba ya fedha za kigeni
Vita vya Sudan: Watu 10 wameuawa katika shambulio la droni kwenye sherehe ya harusi
Wafanyakazi wa afya nchini DR Congo wagoma huku vifo vya Ebola vikikaribia 600
Polisi na jeshi la Afrika Kusini wawakamata zaidi ya wachimbaji madini haramu 200
Rais Mnangagwa apitisha sheria ya kumuongezea muda wa kukaa madarakani
Ufaransa yawaondoa wanadiplomasia kutoka Burkina Faso.
Saba Saba: Polisi wapiga marufuku maandamano katika kumbukumbu ya maandamano ya Kenya.
Wakulima wa Uganda wafungua kesi dhidi ya mradi wa bomba la mafuta unaoungwa mkono na Uingereza