| Swahili
UTURUKI
2 dk kusoma
Uturuki yatangaza timu ya wachezaji 26 kwa ajili ya Kombe la Dunia la FIFA 2026
Kocha Vincenzo Montella ametaja kikosi mseto cha wachezaji wa kimataifa na vipaji vinavyoibuka nchini wakati Uturuki ikijiandaa kwa michuano yake ya kwanza katika Kombe la Dunia tangu 2002 ambayo wenyeji ni Marekani, Canada na Mexico.
Uturuki yatangaza timu ya wachezaji 26 kwa ajili ya Kombe la Dunia la FIFA 2026
[MAKTABA] Uturuki itacheza mechi yake ya ufunguzi ya Kombe la Dunia dhidi ya Australia Juni 14 katika uwanja wa BC Place mjini Vancouver. / AA

Uturuki imetangaza kikosi cha wachezaji 26 kwa ajili ya fainali za Kombe la Dunia la FIFA 2026, huku kocha Vincenzo Montella akichagua mseto wa wachezaji wa kimataifa wenye uzoefu na vipaji viinavyoibuka kwa ajili ya mashindano hayo yatakayochezwa Marekani, Canada, na Mexico.

Mechi hizo zitaanza Juni 11 hadi Julai 19, Uturuki ikirudi tena kwenye michuano ya Kombe la Dunia baada ya kufuzu kupitia mashindano ya Ulaya.

Nahodha Hakan Calhanoglu anaongoza kikosi hicho, pamoja na mchezaji mahiri wa Real Madrid Arda Guler, mshambuliaji wa Juventus Kenan Yildiz na mlinzi Merih Demiral.

Montella amewaita magolikipa watatu: Altay Bayindir, Mert Gunok na Ugurcan Cakir.

Safu ya ulinzi, Abdulkerim Bardakci, Eren Elmali, Caglar Soyuncu, Mert Muldur, Ferdi Kadioglu, Merih Demiral, Ozan Kabak, Samet Akaydin na Zeki Celik wamechaguliwa.

Nafasi ya kiungo inajumuisha Hakan Calhanoglu, Ismail Yuksek, Kaan Ayhan, Orkun Kokcu na Salih Ozcan.

Safu ya mashambulizi Uturuki ina Arda Guler, Baris Alper Yilmaz, Yunus Akgun, Can Uzun, Deniz Gul, Irfan Can Kahveci, Kenan Yildiz, Kerem Akturkoglu na Oguz Aydin.

Baadhi ya wachezaji makinda, ikiwemo Can Uzun na Deniz Gul, pia wamejumuishwa kwenye kikosi cha mwisho huku Uturuki ikijiandaa kuonesha tena umahiri wake chini ya kocha Montella.

Ratiba ya mechi

Uturuki itaanza mechi zake za Kombe la Dunia dhidi ya Australia Juni 14 katika uwanja wa BC Place mjini Vancouver.

Nyota hao wa Hilali kisha watapambana na Paraguay Juni 20 huko San Francisco Bay kabla ya kukabiliana na wenyeji Marekani Juni 26 huko Los Angeles.

Ratiba ya mechi za Uturuki (GMT):

• Juni 14: Australia vs. Uturuki – 0400 (Vancouver)
• June 20: Uturuki vs. Paraguay – 0300 (San Francisco Bay Area)
• June 26: Uturuki vs. Marekani – 0200 (Los Angeles)

Uturuki inalenga kupita zaidi ya hatua ya makundi na kufanikiwa zaidi ya historia waliyoiweka 2002 ambapo walimaliza nafasi ya tatu katika Kombe la Dunia la FIFA.

CHANZO:AA
Soma zaidi
Amani nchini Ukraine ni muhimu kwa usalama na utulivu wa kikanda: Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki
Uturuki na India waweke 'tofauti zao kando' na kuangazia agenda chanya: Fidan
Emine Erdogan: Taka Sifuri nguzo muhimu ya hatua ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi
Nini kitarajiwe kutoka kwa ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Hakan Fidan nchini Bangladesh
Trump kuhudhuria 'mkutano muhimu' wa NATO nchini Uturuki: Rubio
Uturuki, Armenia wafanya mkutano wa biashara Kars kuimarisha uhusiano wa kiuchumi
Spika wa bunge la Uturuki ashtumu UN kutokuwa 'thabiti' katika kuzuia migogoro
Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Hakan Fidan awasili Indonesia ili kuimarisha uhusiano wa kibiashar
Usambazaji wa gesi wa Uturuki, Azerbaijan nchini Syria kutasaidia maendeleo, usalama: Rais Erdogan
Mfumo wa kizazi kijacho wa Uturuki wa BLUEVISION waboresha usalama wa usafiri wa baharini
Erdogan aadhimisha kumbukumbu ya miaka 573 ya ushindi wa Istanbul, anatoa heshima kwa Mehmed II
Uturuki yawakumbuka waliouawa kwenye mashambulizi ya ubaguzi wa rangi ya Solingen 1993
Erdogan aadhimisha Eid al-Adha na ujumbe wa mshikamano wa Gaza, amkemea 'mnyanyasaji' Netanyahu
Erdogan aadhimisha Eid al-Adha kwa ujumbe wa umoja Gaza, amkashifu "muuaji" Netanyahu
Israel inaendelea na uvamizi na mauaji Gaza na Lebanon licha ya makubaliano ya kusitisha mapigano
Uturuki na nchi nyengine 7 zalaani udhalilishaji wa Israel dhidi ya wanaharakati wa Flotilla
Wataalamu wanakusanyika katika Jukwaa la Afrika 2026 ili kujadili uhusiano kati ya Uturuki na Afrika
Idara ya Ujasusi ya Uturuki yanasa washukiwa 10 wa Daesh katika operesheni ya Syria
Uturuki imekuwa kitovu cha nishati, mtetezi wa amani huku kukiwa na mvutano wa kikanda: Rais Erdogan
Erdogan wa Uturuki asisitiza kuunga mkono uhuru wa Sudan katika mazungumzo na Waziri Mkuu Idris