Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan siku ya Jumanne aliwasili jijini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, kwa ziara rasmi.
Erdogan na ujumbe wake walilakiwa na Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed, Waziri wa Mambo ya Nje Gedion Timothewos, na Balozi wa Uturuki nchini Ethiopia Berk Baran katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole jijini Addis Ababa.
Abiy alieleza “kufurahishwa kwake kwa dhati katika kumlaki” Erdogan “Kwenye Ardhi ya Asili ya binadamu” kwenye ujumbe aliouweka katika mtandao wa kijamii wa Marekani X.
Alieleza kuwa kutembeleana kunaweka msisitizo katika “nguvu ya ushirikiano thabiti” kati ya Uturuki na Ethiopia.
“Kutoka Ankara hadi Addis Ababa, natarajia kuwa na majadiliano yenye tija ambayo yataimarisha zaidi ushirikiano na kutilia nguvu uhusiano kati ya nchi hizi mbili za tangu enzi,” waziri mkuu aliongeza.
Abiy alieleza kuwa ni “fahari” kuwa na Erdogan kumuonesha “ukarimu” wa Ethiopia, akiitaja nchi yake kuwa “sehemu ambayo huwezi kujihisi mgeni lakini kama rafiki wa dhati.”
Aliongeza kuwa wawili hao wanaweza kunywa “kahawa ambayo iligunduliwa mara ya kwanza kwenye ardhi hiyo” huku wakijadili masuala na kuimarisha “ushirikiano uliokita mizizi kutokana na fursa zinazojitokeza kwa ushirikiano wetu.”














