Uongozi wa Burkina Faso umeagiza kufutwa kwa mashirika karibu 200.
Kwa ujumla, nchi hiyo ya Sahel imesimamisha shughuli za mashirika 205, yote yenye kuhusika katika sekta ya afya, elimu, haki za wanawake, kilimo, mazingira, utamaduni na michezo.
Julai 2025, Rais wa mpito Kapteni Ibrahim Traore alitia saini sheria ya masharti makali kwa mashirika ya haki za binadamu pamoja na mengine.
ZILIZOPENDEKEZWA
"Kipindi cha kusitishwa kwa muda, yale ambayo yatahakikisha mashirika yanaheshimu sheria ndiyo yataruhusiwa," serikali imesema kwenye agizo.
Mashirika yasiyo ya serikali ya kimataifa na yale ya misaada ambayo yanapokea fedha kutoka kwa wafadhili wa nje mara nyingi yanashtumiwa na Burkina Faso kwa ujasusi au kushirikiana na magaidi wanaopigana na jeshi.
CHANZO:TRT Afrika Swahili
















